Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Sheikh Ponda: Nimemwona Lissu, nimeumia
Habari za Siasa

Sheikh Ponda: Nimemwona Lissu, nimeumia

Sheikh Ponda akiwa ndani ya kituo cha televisheni cha Horizon cha nchini Kenya
Spread the love

KATIBU wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Issa Ponda ameueleza mtandao huu kwamba, amefanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania, Tundu Lissu anayendelea na matibabu jijini Nairobi nchini Kenya, anaandika Faki Sosi.

Kiongozi huyo wa dini ametoa kauli hiyo leo baada ya kuulizwa na mtandao huu kuhusu safari na malengo yake nchini Kenya ambapo amesema, ilihusu masuala ya kijamii.

“Nikiwa kwenye safari yangu ya masuala ya kijamii nchini Kenya, nimeonana na Mheshimiwa Lissu hospitalini alikolazwa, nilienda kumjulia hali na kufanya naye mazungumzo.”

Sheikh Ponda amesema “Kwa kweli tukio la Mheshimiwa Lissu linaumiza, nimefanikiwa kumwona, lakini nimepanga kuzungumza na vyombo vya habari nchini kuhusu mazungumzo yangu na Mheshimiwa Lissu kesho (Jumatano), naomba uwe na subra mpaka kesho.”

Kwa uchache Sheikh Ponda amesema, pamoja na kumtembelea Lissu, alipata fursa ya kutembelea Kituo cha Televisheni cha Horizon (HORIZON TV).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!