Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Shabiki wa Yanga atisha, atoka Arusha mpaka Kigoma kwa baiskeli
Michezo

Shabiki wa Yanga atisha, atoka Arusha mpaka Kigoma kwa baiskeli

Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa Fainali wa Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation), Shabiki wa klabu ya Yanga, Iddi Mkuu (69) ametinga Kigoma leo akitokea Arusha kwa kutumia baiskeli kushuhudia mchezo huo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea). 

Mchezo huo ambao utawakutanisha mafahari wawili Simba dhidi ya Yanga, utapigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma tarehe 25 Julai, 2021 kuanzia majira ya saa 10 jioni.

Shabiki huyo ambaye ametumia siku kumi njiani, huku akiendesha baiskeli kwa kilomita Zaidi ya 1,000.

Baada ya kuwasili Kigoma, shabiki huyo wa Yanga alipokelewa kwa shangwe na mashabiki wa klabu hiyo na kumpeleka kwenye moja ya tawi lao.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, shabiki huyo alisema, amekuja kushuhudia fainali hiyo licha ya kukutana na changamoto njiani.

“Nimekuja kushuhudia fainali ya FA hapa kigoma na wakati natoka kule nilipanga nifike hapa ndani ya siku 10.

“Changamoto zipo, kuna wanyama wakali mbugani na nilikutana na Twiga na akanipisha mimi nikaenda zangu,” alisema shabiki huyo.

Safari ya shabiki huyo kutoka mkoani Arusha ilianza jioni ya tarehe 12, siku ya Jumatatu na kufika mkoani Kigoma leo tarehe 21 Julai, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!