Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Shabiki wa Yanga atisha, atoka Arusha mpaka Kigoma kwa baiskeli
Michezo

Shabiki wa Yanga atisha, atoka Arusha mpaka Kigoma kwa baiskeli

Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa Fainali wa Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation), Shabiki wa klabu ya Yanga, Iddi Mkuu (69) ametinga Kigoma leo akitokea Arusha kwa kutumia baiskeli kushuhudia mchezo huo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea). 

Mchezo huo ambao utawakutanisha mafahari wawili Simba dhidi ya Yanga, utapigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma tarehe 25 Julai, 2021 kuanzia majira ya saa 10 jioni.

Shabiki huyo ambaye ametumia siku kumi njiani, huku akiendesha baiskeli kwa kilomita Zaidi ya 1,000.

Baada ya kuwasili Kigoma, shabiki huyo wa Yanga alipokelewa kwa shangwe na mashabiki wa klabu hiyo na kumpeleka kwenye moja ya tawi lao.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, shabiki huyo alisema, amekuja kushuhudia fainali hiyo licha ya kukutana na changamoto njiani.

“Nimekuja kushuhudia fainali ya FA hapa kigoma na wakati natoka kule nilipanga nifike hapa ndani ya siku 10.

“Changamoto zipo, kuna wanyama wakali mbugani na nilikutana na Twiga na akanipisha mimi nikaenda zangu,” alisema shabiki huyo.

Safari ya shabiki huyo kutoka mkoani Arusha ilianza jioni ya tarehe 12, siku ya Jumatatu na kufika mkoani Kigoma leo tarehe 21 Julai, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!