Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sethi amalizana na DPP, kutoka leo
Habari MchanganyikoTangulizi

Sethi amalizana na DPP, kutoka leo

Mwenyekiti Mtendaji wa IPTL, Harbinder Seth
Spread the love

 

MFANYABIASHARA Harbinder Sethi, anayesota rumande kwa takribani miaka minne, akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi, anatarajiwa kutoka baada ya kumalizana na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Sylvester Mwakitalu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 16 Juni 2021 na DPP Mwakitalu, akizungumza na MwanaHALISI Online, kwa simu, kuhusu mwenendo wa kesi hiyo, iliyoko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

DPP Mwakitalu amesema, Sethi huenda akatoka leo, kama atakamilisha taratibu walizokubaliana katika mazungumzo ya makubaliano kisheria (Plea Bagaining), ya kumaliza kesi hiyo, ambayo ilikuwa na washtakiwa wengine wawili, Mfanyabiashara James Rugemalira na Wakili Joseph Makandege.

Mkurugenzi huyo wa mashtaka amesema, alifanya mazungumzo na Sethi, baada ya kupitia upya mwenendo wa kesi hiyo ya uhujumu uchumi Na. 27/2017, iliyofunguliwa mahakamani hapo Juni 2017.

“Kesi ya Sethi tunai-review (pitia, ) lakini Sethi leo atatoka. Leo tunamalizana naye. Mfanyabiashara huyo tumemalizana naye kwa Plea Bargaining, kuna makosa amekiri ataadhibiwa halafu leo atatoka,” amesema DPP Mwakitalu.

Hata hivyo, DPP Mwakitalu hakuweka bayana makubaliano yake na Sethi, kuhusu kumaliza kesi hiyo, akisema kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, itatoa taarifa zaidi kama itafikia uamuzi wa kumuacha huru mfanyabiashara huyo.

Sethi na wenzake wawili, wanakabiliwa na mashtaka 12 katika kesi hiyo, ikiwemo utakatishaji fedha, kula njama na kujihusisha na mtandao wa uhalifu.

Mengine ni, kughushi na kutoa nyaraka za kughushi na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, pamoja na kusababisha hasara kwa Serikali, zaidi ya Dola za Marekani 22 milioni na Sh, 309.46 bilioni.

Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo, kati ya tarehe 18 Oktoba 2011 na tarehe 19 Machi 2014, jijini Dar es Salaam.

Sethi na wenzake wanadaiwa kujipatia fedha kinyume cha sheria, katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwa ajili ya utekelezaji wa mkataba wa ununuzi wa umeme na umiliki wa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!