Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali Z’bar yafuta kongamano la maridhiano
Habari za SiasaTangulizi

Serikali Z’bar yafuta kongamano la maridhiano

Dk. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar (kushoto) walipokuwa katika mazungumzo ya muafaka na Maalim Seif Shariff Hamad
Spread the love

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imefuta kongamano la kimataifa la kujadili mustakbali wa maridhiano Zanzibar lililokuwa lifanyike kesho. Anaripoti Jabir Idrissa, Zanzibar … (endelea).

Kongamano hilo ambalo lingeshirikisha watu kadhaa mashuhuri na wasomi wa Tanzania na nje ya nchi, limeandaliwa na Kituo cha Katiba cha Afrika Mashariki, asasi ya kitafiti inayojumuisha wanasheria mabingwa katika kanda ya Afrika Mashariki.

Ilikuwa ni matarajio ya wananchi hapa kwamba kupitia kongamano hilo wangepata taarifa za namna gani Zanzibar inaweza kuondokana na migogoro ya kisiasa na hasa huu unaoidhoofisha nchi kwa kuwa imegawanyika kutokana na kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba 2015 uliokuwa umeonesha kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kilishindwa na Chama cha Wananchi (CUF).

Tangazo la kufutwa kwa kongamano lilitolewa ghafla jioni na halikuwa na ufafanuzi zaidi ya kusema, “tunaomba radhi kwa usumbufu uliosababishwa na taarifa yetu.”

Waandaaji wake wameiambia MwanahalisiOnline kuwa tangazo limetoka baada ya kikao kilichosimamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib, Ayoub Mohamed Mfaume ambaye amenukuliwa akisema hali ya usalama inaweza kuharibika iwapo kongamano litaruhusiwa kufanyika.

Ayoub ambaye kwa nafasi yake ndiye mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa, ametoa msimamo huo mbele ya waandaaji wa kongamano kwenye Hoteli ya DoubleTree by Hilton ya mjini hapa.

Kongamano lenyewe lilikusudia kuzungumzia mapendekezo ya kituo baada ya kufanya utafiti wa hali mbaya ya kisiasa iliyopo Zanzibar kutokana na kuvunjwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyokuwa imeundwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2010.

Baada ya uchaguzi kufutwa kinyemela kwa tangazo la Jecha Salim Jecha aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kulifanywa kilichoitwa “uchaguzi wa marudio” ambao matokeo yake ni Dk. Ali Mohamed Shein wa CCM, kutangazwa mshindi wa zaidi ya asilimia 90.

Aliunda serikali isiyokuwa na muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na mpaka sasa ndiyo inayoendelea kuongoza huku CUF ikiipinga kwa kutoitambua.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!