Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali Z’bar yafuta kongamano la maridhiano
Habari za SiasaTangulizi

Serikali Z’bar yafuta kongamano la maridhiano

Dk. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar (kushoto) walipokuwa katika mazungumzo ya muafaka na Maalim Seif Shariff Hamad
Spread the love

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imefuta kongamano la kimataifa la kujadili mustakbali wa maridhiano Zanzibar lililokuwa lifanyike kesho. Anaripoti Jabir Idrissa, Zanzibar … (endelea).

Kongamano hilo ambalo lingeshirikisha watu kadhaa mashuhuri na wasomi wa Tanzania na nje ya nchi, limeandaliwa na Kituo cha Katiba cha Afrika Mashariki, asasi ya kitafiti inayojumuisha wanasheria mabingwa katika kanda ya Afrika Mashariki.

Ilikuwa ni matarajio ya wananchi hapa kwamba kupitia kongamano hilo wangepata taarifa za namna gani Zanzibar inaweza kuondokana na migogoro ya kisiasa na hasa huu unaoidhoofisha nchi kwa kuwa imegawanyika kutokana na kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba 2015 uliokuwa umeonesha kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kilishindwa na Chama cha Wananchi (CUF).

Tangazo la kufutwa kwa kongamano lilitolewa ghafla jioni na halikuwa na ufafanuzi zaidi ya kusema, “tunaomba radhi kwa usumbufu uliosababishwa na taarifa yetu.”

Waandaaji wake wameiambia MwanahalisiOnline kuwa tangazo limetoka baada ya kikao kilichosimamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib, Ayoub Mohamed Mfaume ambaye amenukuliwa akisema hali ya usalama inaweza kuharibika iwapo kongamano litaruhusiwa kufanyika.

Ayoub ambaye kwa nafasi yake ndiye mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa, ametoa msimamo huo mbele ya waandaaji wa kongamano kwenye Hoteli ya DoubleTree by Hilton ya mjini hapa.

Kongamano lenyewe lilikusudia kuzungumzia mapendekezo ya kituo baada ya kufanya utafiti wa hali mbaya ya kisiasa iliyopo Zanzibar kutokana na kuvunjwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyokuwa imeundwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2010.

Baada ya uchaguzi kufutwa kinyemela kwa tangazo la Jecha Salim Jecha aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kulifanywa kilichoitwa “uchaguzi wa marudio” ambao matokeo yake ni Dk. Ali Mohamed Shein wa CCM, kutangazwa mshindi wa zaidi ya asilimia 90.

Aliunda serikali isiyokuwa na muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na mpaka sasa ndiyo inayoendelea kuongoza huku CUF ikiipinga kwa kutoitambua.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!