Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali: Z’bar hakuna corona
Afya

Serikali: Z’bar hakuna corona

Zanzibar
Spread the love

 

SERIKALI ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar (SUK), imeeleza, hakuna mgonjwa yeyote wa corona visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Mansor Mazrui, Waziri wa Afya wa Zanzibar jana tarehe 22 Juni 2021, katika mahojiano na Kituo cha Utangazaji cha Uingereza (BBC).

“Nikuthibitishie kwamba Zanzibar hatuna mgonjwa hata mmoja wa corona, wodi zetu zipo wazi. Sisi bado hatupimi corona hapa kwa wageni wanaaoingia nchini, tunapima wakati wa kutoka nchini.”

“Kwa sababu wakati wa kutoka wanahitajia mashirika ya ndege ili wakiondoka waoneshe certificate (vyeti) zao, lakini wanaokuja nchini hapa wanakuja na certificate zao. Kwa hiyo watu wote wanaokuja hapa wanakuja na certificate zao zinazoonesha negative (hawana).”

Mazrui amesema, kutokana na utaratibu wa wa wageni kuingia viswani humo nav yeti vyao vinavyoonesha hawana virusi hivyo, Zanzibar mpaka sasa haina rekodi yoyote ya maambukizi hayo.

Amesema, “kwa hiyo, mpaka sasa hatuna mgonjwa hata mmoja wa COVD-19 Zanzibar, si raia si mzanzibari yeyote kutoka nje, bado hatujapokea kesi hiyo.”

Tanzania ambapo Zanzibar ni sehemu yake, imewatangazia wananchi wake kuchukua tahadhari zaidi kuhusu wimbi la tatu la virusi vya corona.

Kutokana na hatua hiyo, baadhi ya maeneo ya mkusanyiko tayari yametoa tahadhari na ulazima wa kuvaa barako, miongoni mwayo ni Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!