Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaunda kikosi kukabili wanyamapori waharibifu
Habari Mchanganyiko

Serikali yaunda kikosi kukabili wanyamapori waharibifu

Mary Masanja nail Waziri wa Maliasili na utalii
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeunda kikosi maalum kitachoshirikiana na wadau mbalimbali, kwa ajili ya kudhibiti wanyamapori wakali na wahalibifu katika maeneo yanayozunguka hifadhi. Anaripoti Nasra Bakari, DMC…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja, leo Jumatatu tarehe 10 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi, Morogoro.

“Je, serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Wananchi wanaoishi kwenye vijiji vinavyopakana na hifadhi pamoja na mali zao, wanakuwa salama kwani wanyamapori wamekuwa wakiingia na kufanya uharibifu kwenye vijiji,” amehoji Londo.

Waziri Masanja amesema, serikali inatambua vijiji vinavyozunguka hifadhi za wanyamapori nchini, vinakabiliwa na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu kama vile Tembo, Simba, Nyati, Viboko na Mamba.

Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi

Amesema, katika kupambana na wanyamapori hawa, serikali imeunda kikosi maalum cha kupambana nao, hususani kwenye maeneo yanayozunguka hifadhi kwa kadri taarifa za matukio zinavyopatikana.

“Aidha, serikali imeandaa mpango mkakati wa kitaifa wa kushughulikia wanyamapori wakali na wahalibifu, ambao unatoa mwongozo wa namna nzuri ya kuwawezesha wananchi kutumia maeneo yao bila kuathiriwa, mikakati hiyo ni pamoja na;-

Kutoa mafunzo kwa wananchi wanaoishi maeneo ya pembezoni mwa hifadhi kuhusu mbinu bora za kukabiliana na wanyamapori wakali na wahalibifu, mafunzo haya ni endelevu na yatafanyika katika maeneo yote yenye changamoto.

Pia kuimarisha vikosi vya doria za kudhibiti wanyamapori vikiwemo vitendea kazi ili viweze kufanya doria na kushirikiana na Halmashauri za wilaya na vijiji ili kuwezesha uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi.

Masanja amesema, Wananchi wa Mikumi na maeneo mengine yanaozunguka hifadhi, waendelee kutoa ushirikiano na
kufuata maelezo ya wataalam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!