Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali yatoa Sh. 573 mil. kukamilisha wa ujenzi sekondari ulioanzishwa na wanakijiji
Elimu

Serikali yatoa Sh. 573 mil. kukamilisha wa ujenzi sekondari ulioanzishwa na wanakijiji

Spread the love

 

SERIKALI kupitia Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga Sh. 573 milioni, kwa ajili ya ujenzi wa Sekondari ya Wanyere, wilayani Musoma Vijijini, Mkoa wa Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, katika mkutano wake na wanakijiji cha Wanyere, uliofanyika jana Jumatano.

“Bajeti ya 2023/24, Serikali itatoa Sh. 573 milioni kupitia mradi wake wa SEQUIP kwa ajili ya ujenzi wa Sekondari mpya katika Kijiji cha Wanyere. Hii itakuwa shule ya pili katika Kata ya Suguti,” amesema Prof. Muhongo.

Prof. Muhongo ameishukuru Serikali ya Rais Samia, kwa kuendelea kutoa fedha za kuboresha miundombinu ya elimu jimboni humo, huku akitaka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, kutoa fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya kuboresha sekta hiyo.

Amesema fedha hizo zilizopangwa kutolewa na Serikali, zitaunga mkono juhudi za wananchi walioanza kujenga shule hiyo kwa nguvu na fedha zao.

Prof. Muhongo amesema, hadi sasa amechangka mifuko 100 ya saruji, wakati wananchi wakichagia Sh. 2. 5 milioni, saruji mifuko 30, pamoja na nguvu kazi.

“Kwa sasa wanakijiji cha Wanyere wanalazimika kutembea zaidi ya kilomita 30 kwenda na kurudi kutoka masomoni kwenye sekondari ya kata. Baadhi yao wamepanga vyumba na wanajipikia karibu na eneo la shule, hivyo shule hii ikikamilika itasaidia kuondoa changamoto hizo,” amesema Prof. Muhongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

Elimu

Takukuru wambana Mwalimu mkuu, atema bungo

Spread the loveMwalimu Mkuu wa shule msingi Hanihani, kata ya Igunga wilayani...

error: Content is protected !!