Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali yatoa muongozo waliokimbia shule kurejea
Elimu

Serikali yatoa muongozo waliokimbia shule kurejea

Prof Adolf Mkenda, Waziri wa Elimu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imetoa muongozo na utaratibu wa wanafunzi walioacha masomo kwa sababu mbalimbali, kurudi shuleni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 9 Machi 2022, jijini Dar es Salaam na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolph Mkenda, akitoa taarifa ya mafanikio ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan, madarakani.

“Maagizo ya Rais ni kuhakikisha wote wanaweza kurudi na kumalizia masomo yao na hilo tayari wizara imeshatolea muongozo na utaratibu wa namna ya kurudi na natumia fursa hii tena kuwahimiza watoto walaiocha shule kuna fursa ya kurudi,” amesema Prof. Mkenda.

Waziri huyo wa elimu, amesema wanafunzi wanaotaka kurejea kwa mwalimu mkuu wa shule waliyokuwa wanasoma, ambapo kuna muongozo wa kamishna wa elimu unaoelezea utaratibu wa namna ya kurudi kwenye masomo.

Prof. Mkenda amesema, Rais Samia ana lengo la kuhakikisha watoto wote wanapata elimu, ikiwemo wale waliokatisha masomo kwa sababu ya kupata ujauzito wakiwa shuleni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!