Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Serikali yatoa leseni mpya za madini
Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa leseni mpya za madini

Spread the love

LESENI mpya za madini takribani 7,879 zimetolewa na Tume ya Madini kuanzia mwezi Mei hadi Septemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wake na wanahabari uliofanyika leo tarehe 4 Oktoba 2018 jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema leseni hizo zimetolewa baada ya maombi yake kupitishwa na kikao cha tume hiyo kilichofanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu.

Akichanganua kuhusu leseni hizo, Prof. Kikula ameeleza kuwa, leseni za utafutaji wa madini zilizotolewa ni 263, leseni kubwa mpya zilizotolewa ni 3, leseni za uchimbaji wa kati 14 na leseni 1 ya sihia ya uchimbaji wa kati.

Prof. Kikula ameeleza kuwa, maombi ya leseni za uchimbaji wa kati 14 yaliyopitishwa yaliwasilishwa na kampuni za Dangote Industries Limited kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya chokaa katika eneo la Mtwara; Nazareth Mining Investment Co Limited kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya kinywe (graphite) katika eneo la Ruangwa mkoani Lindi na kampuni ya Sunshine Mining (T) Limited kwa ajili ya uchimbaji wa madini dhahabu katika eneo la Chunya mkoani Mbeya.

Aidha, Prof. Kikula amesema Tume imeweka mikakati ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini kwa kuwatengea maeneo maalum kwa ajili ya uchimbaji madini, ambapo amewataka kuunda vikundi na kusajiliwa kupitia viongozi wao hivyo kuwezesha upatikanaji wa leseni za madini na kufanya shughuli zao pasipo kikwazo chochote.

“Sisi kama Tume ya Madini tunatambua mchango mkubwa wa wachimbaji wadogo wa madini na ndio maana tumekuwa tukifanya ziara katika maeneo ya wachimbaji wadogo na kutatua changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na migogoro; tunataka wafanye kazi katika mazingira salama kabisa,” alisema Profesa Kikula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!