Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yatoa leseni mpya za madini
Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa leseni mpya za madini

Spread the love

LESENI mpya za madini takribani 7,879 zimetolewa na Tume ya Madini kuanzia mwezi Mei hadi Septemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wake na wanahabari uliofanyika leo tarehe 4 Oktoba 2018 jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema leseni hizo zimetolewa baada ya maombi yake kupitishwa na kikao cha tume hiyo kilichofanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu.

Akichanganua kuhusu leseni hizo, Prof. Kikula ameeleza kuwa, leseni za utafutaji wa madini zilizotolewa ni 263, leseni kubwa mpya zilizotolewa ni 3, leseni za uchimbaji wa kati 14 na leseni 1 ya sihia ya uchimbaji wa kati.

Prof. Kikula ameeleza kuwa, maombi ya leseni za uchimbaji wa kati 14 yaliyopitishwa yaliwasilishwa na kampuni za Dangote Industries Limited kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya chokaa katika eneo la Mtwara; Nazareth Mining Investment Co Limited kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya kinywe (graphite) katika eneo la Ruangwa mkoani Lindi na kampuni ya Sunshine Mining (T) Limited kwa ajili ya uchimbaji wa madini dhahabu katika eneo la Chunya mkoani Mbeya.

Aidha, Prof. Kikula amesema Tume imeweka mikakati ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini kwa kuwatengea maeneo maalum kwa ajili ya uchimbaji madini, ambapo amewataka kuunda vikundi na kusajiliwa kupitia viongozi wao hivyo kuwezesha upatikanaji wa leseni za madini na kufanya shughuli zao pasipo kikwazo chochote.

“Sisi kama Tume ya Madini tunatambua mchango mkubwa wa wachimbaji wadogo wa madini na ndio maana tumekuwa tukifanya ziara katika maeneo ya wachimbaji wadogo na kutatua changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na migogoro; tunataka wafanye kazi katika mazingira salama kabisa,” alisema Profesa Kikula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!