Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali yatenga Bilioni 8 kwa watoto wa kaya masikini
ElimuHabari za Siasa

Serikali yatenga Bilioni 8 kwa watoto wa kaya masikini

Spread the love

 

SERIKALI imetenga Sh. 8 bilioni kwa ajili ya kuanzisha dirisha maalumu (Special Fund) litakalokuwa linasaidia watoto wanaotoka katika familia masikini. Anaripoti Erasto Masalu, Dar es Salaam … (endelea).

Akisoma Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2022/2023, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema dirisha hilo litaanzishwa chini ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia masikini.

Dk. Mwigulu amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameamua kuanzisha dirisha hilo kupitia Tasaf baada ya kuguswa na watoto wanaokatisha masomo kwasababu mbalimbali ikiwemo kushindwa kupata mahitaji muhimu.

Waziri huyo alisema pamoja na serikali kuendelea kugharamia programu ya elimu msingi bila ada lakini wanafunzi wanakatisha masomo yao kutokana na umasikini wa kipato kwenye familia zao, mimba za utotoni, mwamko duni wa elimu kwa baadhi ya jamii na utoro na wale wasioendelea kwa mujibu wa sheria (Ufaulu).

Waziri wa Fedha na Mpango wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba

“Ili kukabiliana na utoro (drop out) wa wanafunzi wanaotoka familia masikini, bado tuna watoto wanaoshindwa kumudu mahitaji ya lazima licha ya kuwepo kwa programu ya elimu bila malipo na hivyo wanasaidiwa na wabunge, madiwani na wengine kuchangiwa na wasamaria wema,” amesema Waziri Nchemba.

Waziri Nchemba amesema dirisha hilo litakuwa chini ya Tasaf kutokana na wao kuwa na mfumo wa kanzi data (database) ya watoto masikini wanaopatikana katika shughuli zao za kila siku.

Pia Waziri Nchemba amesema mbali na kanzidata ya TASAF watashirikiana na taarifa za wabunge na madiwani kutoka katika maeneo husika kupata watoto wanaotoka katika kaya masikini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!