Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Serikali yataka Ma  RC ,  Ma  Dc wasijione  ‘miungu watu’
Habari Mchanganyiko

Serikali yataka Ma  RC ,  Ma  Dc wasijione  ‘miungu watu’

Selemani Jafo, Waziri wa Nchi ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

WAKUU wa Mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya nchini wametakiwa kutumia vizuri sheria ya kwaweka ndani watu ndani ya saa 48 na wasitumie sheria hiyo kwa kuwaonea watu, anaandika Dany Tibason.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Nchi,Ofisi ya Rais (TAMISEMI)Selemani Jaffo alipokuwa akifunga mafunzo ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wao kwa lengo la kuwajengea uwezo.

Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi, Jaffo amesema kwa sasa kuna baadhi yao  wanatumia vibaya sheria inayowapa  mamlaka ya kumuweka ndani mtu kwa  saa 48.

“Serikali imekua ikichukiwa kutokana na viongozi hawa  kutumia vibaya sheria inayompa mamkala kiongozi huyo kumuweka ndani  mtu mahabusu saa 48.

“Wapo wakuu ambao wanatumia sheria hiyo kwa kukomoana na kujifanya kuwa wao ni miungu watu bila kutambua kuwa wanapofanya hivyo wanasababisha serikali kuchukiwa bila kuwa na sababu za msingi” alisema Jafo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!