Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yataka Ma  RC ,  Ma  Dc wasijione  ‘miungu watu’
Habari Mchanganyiko

Serikali yataka Ma  RC ,  Ma  Dc wasijione  ‘miungu watu’

Selemani Jafo, Waziri wa Nchi ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

WAKUU wa Mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya nchini wametakiwa kutumia vizuri sheria ya kwaweka ndani watu ndani ya saa 48 na wasitumie sheria hiyo kwa kuwaonea watu, anaandika Dany Tibason.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Nchi,Ofisi ya Rais (TAMISEMI)Selemani Jaffo alipokuwa akifunga mafunzo ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wao kwa lengo la kuwajengea uwezo.

Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi, Jaffo amesema kwa sasa kuna baadhi yao  wanatumia vibaya sheria inayowapa  mamlaka ya kumuweka ndani mtu kwa  saa 48.

“Serikali imekua ikichukiwa kutokana na viongozi hawa  kutumia vibaya sheria inayompa mamkala kiongozi huyo kumuweka ndani  mtu mahabusu saa 48.

“Wapo wakuu ambao wanatumia sheria hiyo kwa kukomoana na kujifanya kuwa wao ni miungu watu bila kutambua kuwa wanapofanya hivyo wanasababisha serikali kuchukiwa bila kuwa na sababu za msingi” alisema Jafo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!