Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yarejesha ununuzi wa mazao kwa vyama vya ushirika
Habari Mchanganyiko

Serikali yarejesha ununuzi wa mazao kwa vyama vya ushirika

Waziri wa Kilimo Tanzania, Hussein Bashe
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imerejesha mfumo wa zamani wa ununuzi wa mazao ya kimkakati, ili kuondoa changamoto za mfumo wa soko huria. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe18 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu waziri wa Kilimo, Hussen Bashe, akimjibu Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa mkoani Kagera, aliyehoji mkakati wa Serikali katika kutatua changamoto ya ucheleweshaji malipo kwa wakulima wa kahawa.

Akijibu swali hilo, Bashe amesema baada ya mabadiliko hayo, wakulima watauza mazao yao kupitia vyama vyao vya ushirika.

“Kutokana na changamoto za mfumo wa soko huria, Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kurejesha ununuzi wa mazao matano ya kimkakati (Korosho, Tumbaku, Pamba, Kahawa na Chai), kupitia Vyama vya Ushirika ili kunufaisha wakulima, wanunuzi , wafanyabiashara na Serikali kwa ujumla,” amesema Bashe.

Zao la Korosho

Kuhusu changamoto ya wakulima wa Kahawa mkoani Kagera kuchelewa kulipwa fedha zao, Bashe amevitaka Vya vya Ushirika (AMCOS), kutafuta masoko ya uhakika mapema ili kuondoa changamoto hiyo.

“Katika mfumo wa soko la kahawa Serikali hainunui kahawa bali imeweka mfumo wezeshi kwa wakulima kuuza mazao yao kupitia mfumo wezeshi wa wakulima kuuza mazao yao kupitia mfumo wa ushirika ambapo wanunuzi binafsi wameruhusiwa kununua kahawa kupitia AMCOS,” amesema Bashe na kuongeza:

“Mwongozo wa Bodi ya Kahawa unaelekeza kuwa wakulima walipwe ndani ya siku tatu pindi AMCOS inapofanya makubaliano na kampuni yenye leseni ya kununua kahawa.

Aidha, Vyama vya Ushirika vimeshauriwa Kutafuta masoko mapema ili kuwezesha kupata fedha kutoka taasisi za fedha ikiwemo Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) au wanunuzi wanaoingia nao mikataba ili kuwezesha kulipa wakulima pindi wanapoleta kahawa kwenye Vyama vyao vya msingi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!