Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Serikali yapongeza uwekezaji KHEN sekta elimu ya afya
Habari

Serikali yapongeza uwekezaji KHEN sekta elimu ya afya

Spread the love

 

SERIKALI nchini Tanzania imepongeza uwekezaji uliofanywa na Mtandao wa Elimu ya Afya Kairuki (KHEN), kwenye sekta ya elimu ya afya kwani unachangia juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya afya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar….(endelea)

Pongezi hizo zilitolewa jana Alhamisi tarehe 9 Juni na Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel, wakati wa kongamano la kisayansi lililofanyika kwenye Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert kairuki (HKMU), Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri amesema uwekezaji uliofanywa na Hayati Profesa Kairuki kwenye sekta ya afya ni mkubwa na wa kuigwa kwani umesaidia kupunguza msongamano kwenye hospitali za serikali.

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel, akimsilikiza Maryam Baba wa Kampuni ya TUNZAA alipokwenda kufungua kongamano la kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU)

Amesema Mtandao huo umekuwa na mchango mkubwa kwenye sekta ya afya kwa kuanzisha Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), ambacho kimekuwa kikitoa idadi kubwa ya wataalamu wa sekta ya afya.

“Sayansi ndiyo jicho la taifa lolote duniani hivyo mchango wenu kwenye kuzalisha watalamu wa afya ni mkubwa sana na serikali inathamini kazi kubwa mnayofanya serikali itaendelea kuwasaidia na kuwaunga mkono,” amesema Dk. Mollel.

Amesema Serikali itaendelea kuwekeza kwenye sekta ya afya na tayari Rais Samia Suluhu Hassan ameshatoa Sh bilioni nne kwa Taasisi ya Utafiti wa Afya (NIMRI), ili waweze kutafuta chanjo za kukabiliana na magonjwa mbalimbali.

Amesema wanasayansi lazima wajipange kukabiliana na magonjwa yatokanayo na virusi kwani dalili zinaonyesha kwamba ndilo tishio kubwa duniani kwa siku zijazo.

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel, akiangalia mabango yanayozungumzia maradhi mbalimbali wakati wa kongamanao la kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU)

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Yohana Mashalla, amesema magonjwa ya kuambukiza yamekuwa changamoto kubwa sana kwa nchi zinazoendelea kulinganisha na zile zilizoendelea.

Amesema mlipuko wa ugonjwa wa COVID 19 umeonyesha ni kwa namna gani taifa linapaswa kuweka mifumo imara kujiandaa kukabiliana na majanga ya aina hiyo yatakapotokea siku za mbele.

“Iko haja ya kuimarisha mifumo yetu ya afya ili tuweze kujitayarisha kukabiliana na maradhi ya mlipuko kama COVID 19 na lazima tufahamu kuwa COVID siyo ya kwanza na wala siyo ya mwisho kuna milipuko itakuja tujiandae,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!