Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yaongeza kima cha chini mshahara asilimia 23.3
Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaongeza kima cha chini mshahara asilimia 23.3

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameridhia mapendekezo ya nyongeza ya mshahara kwa watumishi wa umma, ambapo kima cha chini kimeongezwa kwa asilimia 23.3. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Zuhura Yunus, leo Jumamosi, tarehe 14 Mei 2022, Serikali imepanga kutumia Sh. 9.7 katika mwaka wa fedha wa 2022/23, kwa ajili ya kugharamia mishahara ya watumishi wote katika Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi na Wakala wa Serikali.

“Hivyo, bajeti ya mishahara ya mwaka 2022/23 ina ongezeko la Sh. 1.59 trilioni, sawa na asilimia 19.51, ikilinganishwa na bajeti ya mwaka wa fedha wa 2021/22,” imesema taarifa ya Zuhura.

Taarifa ya Zuhura imeongeza kuwa, nyongeza hiyo imefanyika kwa kuzingatia pato la taifa (GDP), mapato ya ndani yanayotarajiwa kukusanywa katika mwaka 2022/23 na hali ya uchumi wa ndani na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine, taarifa ya Zuhura imesema Rais Samia amepokea mapendekezo ya kanuni mpya ya Mafao ya Pensheni , yaliyotolewa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), katika sherehe za siku ya wafanyakazi duniani.

“Rais Samia ameridhia na kuilekeza wizara yenye dhamana na masuala ya hifadhi ya jamii kuendelea kushirikiana na TUCTA na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), ili kukamilisha taratatibu za kuhakikisha malipo ya mkupuo ya asilimia 25 yaliyokataliwa na wadau 2018, yanapandishwa hadi asilimia 33,” imesema taarifa ya Zuhura.

1 Comment

  • Hizo sh trilioni mbili zitatoka wapi? Kama si kuongeza kodi basi ni kukopa kutoka nje. Kwa vyovyote vile tumeliwa kwa sababu ni huyu mfanyakazi ndiye atakayelipa atakapokatwa kodi na tozo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!