Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaombwa kusaidia wafugaji Ngamia
Habari Mchanganyiko

Serikali yaombwa kusaidia wafugaji Ngamia

Ally Kuleva mfugaji wa ngamia kutoka kijiji cha Kambi ya Kumi akiwa anamwelekeza jambo ngamia wake wakati wa maonesho ya 88
Spread the love

SERIKALI imeombwa kuwatambua wafugaji wa Ngamia na kusaidia kuwapunguzia gharama za kuwafuga kwa kuwa wana faida zaidi kuliko wanyama wengine, anaandika Dany Tibason.

Maombi hayo yalitolewa na Ally Kuleva ambaye ni mfugaji wa Ngamia, katika maonesho ya Nanenane mkoani Morogoro.

Kuleva anatokea kijiji cha Kambi ya Kumi wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.

Amesema wafugaji wengi wa ngamia wanakumbwa na changamoto mbalimbali ikiwamo ukosefu wa dawa za kuwatibia wanyama hao.

Ameongeza kuwa kwa sasa serikali ni kama haijaweza kutambua na kuboresha ufugaji wa Ngamia kwa kuwa haiwapi kipaumbele wafugaji hao kwani mpaka sasa hata katika madawa ya mifugo huwezi kupata dawa ambayo inaweza kuwatibu wanyama hao.

Ametaja faida ya wanyama hao kuwa ni pamoja na maziwa yake kutumika kwa ajili ya kutibu vidonga vya tumbo, shinikizo la damu pamoja na magonjwa mbalimbali.

Aidha, amesema mkojo wa mnyama huyo pia ni dawa inayotibu ugonjwa wa pumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!