Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yaombwa kuongeza bajeti Mifugo, Uvuvi
Habari za Siasa

Serikali yaombwa kuongeza bajeti Mifugo, Uvuvi

Ng'ombe wakiwa machungoni
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imeombwa kuongeza bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, pamoja na Tume ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, ili zitekeleze majukumu yake ya ufanisi katika kutatua migigoro kati ya wakulima na wafugaji. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo umetolewa peo Jumanne, tarehe 20 Desemba 2022 na mashirika sita yasiyo ya kiserikali (NGO’s), likiwemo la Haki Ardhi, Tanzania Land Alliance na Pingo’s Forum.

Katika tamko la pamoja la taasisi hizo, zimesema ongezeko la bajeti hizo litasaidia ubainishwaji na upimaji wa nyanda za malisho ya wafugaji, na maeneo ya kilimo.

“Bajeti ziongezwe kwa ajili ya ubainishaji na upimaji wa nyanda za malisho, kauli za kutaka mamlaka hizo kutekeleza wajibu wake bila kuziwezesha ni kiini macho na mwendelezo wa matamko yasiyotekelezeka,” imesema tamko la taasisi hizo.

Katika hatua nyingine, taasiai hizo zimeiomba Serikali ianzishe mijadala ya wazi ya wananchi Ili kutafuta suluhisho la migogoro ya ardhi na uhifadhi.

Mashirika yametoa apendekezo hayo yakisema migogoro ya ardhi imeongezeka ambapo wakulima na wafugaji wameathirika nayo hususan wenye mifugo ambao wamepata hasara baada ya kupigwa mnada kwa makosa ya kuingia maeneo yasiyo sahihi Kwa ajili ya malisho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!