Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yaja na waratibu wa umeme vijijini kila jimbo
Habari za Siasa

Serikali yaja na waratibu wa umeme vijijini kila jimbo

Spread the love

 

KATIKA kuimarisha usimamizi wa miradi ya kupeleka umeme vijini, Serikali imesema inakwenda kuajiri waratibu wa miradi ya umeme vijijini kwa kila jimbo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainishwa leo Jumatano tarehe 1 Juni, 2022 na Waziri wa Nishati, Januari Makamba, akiwasilisha bajeti yam waka 2022/2023.

Mbali na kuimarisha usimamizi wa miradi Makamba amesema pia Waratibu watarahisisha upatikani wa taarifa za maendeleo ya miradi hiyo.

“Waratibu hao watakuwa kiungo cha mawasiliano na taarifa kati ya Wabunge, viongozi wa kisiasa, wakandarasi, REA na wadau wengine,” amesema Makamba.

Ameongeza kwa kushirikiana na TANESCO, waratibu hao watakuwa na wajibu wa kutoa taarifa za mara kwa mara kwa viongozi ikiwemo wa Wabunge kuhusu maendeleo ya miradi.

January Makamba, Waziri wa Nishati

Katika hatua nyingine Makamba amesema Serikali imesikia kilio cha muda mrefu cha wananchi wanaoishi katika maeneo ya mijini yenye sifa zinazolingana na vijiji huku wakilipa bei ya kuunganishiwa umeme ya mijini.

“Nataka niwahakikishie kwamba tumesikia kilio chao na tayari tumeunda timu inayojumuisha Wizara ya Nishati, TANESCO na REA.

“Timu hii itazunguka katika miji yote na kuyabaini maeneo hayo kwa kuwashirikisha Waheshimiwa Wabunge wa maeneo husika.

Amesema maeneo yatakayobainishwa na timu hiyo yatajumuishwa kwenye bei ya vijiji yaani Sh. 27,000, “zoezi hili litafanyika nchi nzima na kukamilishwa ndani ya miezi sita.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!