Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yahofiwa kuburutwa ICC
Habari za SiasaTangulizi

Serikali yahofiwa kuburutwa ICC

Roderick Lutembeka, Katibu wa Baraza la Wazee wa Chadema
Spread the love

KAULI za viongozi wa serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa wananchi, zinaweza kusababisha kufikishwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC). Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Hayo yameelezwa leo na Baraza la Wazee wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mbele ya waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Roderick Lutembeka, Katibu wa baraza hilo mbele ya wanahabari amesema kuwa, viongozi wa serikali wanatoa kauli zinazofifisha matumaini ya wananchi na taifa kwa ujumla na zaidi kutia hofu.

Na kwamba, kumekuwepo na malalamiko ya uvunjwaji wa haki jambo ambalo limesababisha malalamiko kwa jamii lakini serikali inajibu malalamiko hayo kwa kubeza huku uhuru wa mawazo ukiendelea kuminywa.

Lutembeka ameeleza kuwea, jumuiya na taasisi za nje zinashuhudia namna serikali ilivyo vinara katika kubana demokrasia na kuvunja sheria za vyama vya siasa huku kauli za kibabe zikitawala dhidi ya vyama vya upinzani na viongozi wake.

Katibu huyo ametoa mfano wa uchaguzi mdogo katika Majimbo ya Siha na Kinpndoni kwamba, kulitawala vitendo vya ukandamizaji mkubwa wa haki za binaadamu jambo ambalo liliibua hisia za malalamiko na kuonewa huku hisia hazi dhidi ya serikali zikitawala.

Pamoja na hivyo, Lutembeka ameeleza mfano wa kifo cha Akwilina Akwilin, aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kilichomkuta wakati wa maandamano ya wafuasi wa Chadema Mkwajuni, Kinondoni.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi na Jeshi la Polisi wakati wafuasi wa Chadema wakiandamana wakidai hati ya viapo vya mawakala wao kwenye uchaguzi mdogo wa Kinondoni. Akwilina hakuwa miongoni mwa waandamanaji, alikuwa kwenye basi ambapo risasi ilimpata akiwa ndani ya daladala.

Akitaja mifano mingine ametaja tukio la kuuawa kwa Daniel John, aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Hananasif, Kinondoni Dar es Salaam. Daniel aliokotwa ameuawa kwenye fukwe za Bahari ya Coco Beach, alikutwa na majeraha na kwamba, matukio hayo na ile mifanyo ya Ben Saanane yanaongeza hofu kwa wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!