Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yagoma kuwalipa fidia waliokutwa vyeti feki kimakosa
Habari za Siasa

Serikali yagoma kuwalipa fidia waliokutwa vyeti feki kimakosa

Naibu Waziri Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kakunda
Spread the love

SERIKALI  imesema hakuna mfanyakazi aliyeondolewa kazini kimakosa katika zoezi la uhakiki wa vyeti feki, zaidi ya kurudishwa kazini. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kakunda alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Ziwani, Nassor Suleiman Omari (CUF), aliyehoji serikali imewarejesha walimu wangapi  kazini ambao wameathirika na kukumbwa na kukutwa na vyeti feki  kimakosa.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri, Kakunda amesema kuwa ni kweli kulikuwepo na manung’uniko kwa baadhi ya watumishi wa sekta ya walimu ambao walikutwa katika mkumbo wa feti kimakosa.

Amesema kuwa walimu hao walikata rufaa na walimu wapatao 1907 walioonekana kuwa waliingizwa kimakosa katika mfumo wa vyeti feki walirudishwa kazini.

Aidha amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17 na mwaka 2017/18 serikali ilifanya uhakikia wa vyeti vya watumishi wa Umma ili kubaini waliokuwa na vyeti halali na waliokuwa na vyeti vya kugushi.

Amesema katika uhakiki huo, jumla ya walimu 3,655 walibainika kuwa na vyeti vya kugushi na walipoteza sifa za kuendelea kuwa watumishi wa Umma.

Mbali na hilo amesema wale wote ambao walibainika kuwa na vyeti feki hata kama walikuwa wanakaribia kustaafu hawatalipwa mafao yoyote kwani serikali imewasemehe kuwashikati kwani watu hao walitakiwa kushitakiwa kwa kosa la jinai.

Naibu Waziri, Kakunda amesema katika harakati za kuziba pengo la walimu waliondolewa kazini, ndani ya miaka miwili serikali imeajiri jumla ya walimu 6495.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!