Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yafuta ada leseni za Youtube kwa wasanii, wanamichezo, wanahabari, kicheko
Habari MchanganyikoMichezo

Serikali yafuta ada leseni za Youtube kwa wasanii, wanamichezo, wanahabari, kicheko

Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye
Spread the love

 

SERIKALI imetoa ahueni kwa vyombo vya habari vya mtandaoni kwa kupunguza malipo ya ada ya leseni ya mwaka na kuwaondolea ada watoa maudhui ya burudani. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumzia mafanikio ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye leo tarehe 14 Machi 2021 jijini Dar es Salaam amesema kuwa watoa maudhui ya burudani hawatatozwa ada.

Waziri Nape amesema Serikali imepitia na kurekebisha kanuni ya leseni ya maudhui ya burudani kwa ajili ya kukuza vipaji.

Ametoa mfano kwa wasanii wanaoweka maudhui ya nyimbo zao mitandaoni hawatalipia ada.

Akifafanau zaidi amesema watoa maudhui ya michezo na mapishi hawatalipa ada hiyo.

Nape ametanabaisha kuwa watoa maudhui ya habari na matukio ya sasa wamepunguziwa malipo ya ada kutoka Sh milioni moja kufika hadi Sh 500,000 na kwamba fomu ya maombi italipwa kwa Sh 50,000 badala ya Sh 100,000.

“Mmepiga kelele muda mrefu, kelele zenu Rais Samia amezisikia” amesema Waziri Nape.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

error: Content is protected !!