Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yafunguka madai ya wanyamapori kutoroshwa kwa ndege
Habari za Siasa

Serikali yafunguka madai ya wanyamapori kutoroshwa kwa ndege

Serengeti
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesema hakuna ndege zinazoingia katika hifadhi za taifa kwa ajili ya kutorosha wanyamapori, bali ndege zinazoingia hifadhini humo hutumiwa na watalii kwa ajili ya kuharakisha usafiri. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika mkutano uliofanyika mtandaoni leo Jumamosi, tarehe 14 Januari 2023, Waziri wa Maliasili na Utalii,Balozi Pindi Chana, amesema viwanja vya ndege vilivyo katika hifadhi za wanyamapori vinalindwa kwa mujibu wa sheria.

“Hakuna mnyama aliyechukuliwa, tuko imara na salama wanyama wetu wanalindwa kisheria truliyojiwekea wenyewe. Naomba Watanzania watulie na taarifa kwamba kuna ndege imekuja imechukuwa wanyama, hakuna mnyama aliyechukuliwa, usafiri huu unaleta watalii kuja kutalii ndiyo maana tumeweka viwanja vya ndege,” amesema Balozi Pindi.

Balozi Pindi amesema, Serikali inalinda wanyamapori kwa mujibu wa sheria za nchi na mikataba ya kimataifa ambapo kwa sasa imeanza kufunga vifaa maalum vya kufuatilia mienendo yao wawapo hifadhini.

“Wanyama wetu wako salama na baadhi ya maeneo tumeanza kufunga vifaa tuna-watrack wanyama ikiwa pamoja na Tembo, tumetoka kwenye sensa ya wanyama Tanzania ni eneo ambalo lina nyati wengi ndani ya Afrika na ukiwa na nyati wengi ni uhakika wa chakula cha Simba ndiyo maana tuko juu, wizara tukasema tuwe na Jeshi la Uhifadjhi kulinda wanyama,” amesema Balozi Pindi.

Kauli hiyo ya Balozi Pindi Chana imekuja bnaada ya kuibuka taarifa katika mitandao ya kijamii, iliyodai kwamba kuna ndege imeingia kuchukua wanyama kwa ajili ya kuwapeleka nje.

1 Comment

  • Hakuna viwanja vya ndege kwenye hifadhi za Ulaya, Asia wala Amerika. Kwa nini Afrika tunababaishwa kama shamba la bibi? Watumie magari kwa sababu wanaenda kuangalia asilia siyo miji.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!