UHURU wa vyombo vya habari hapa nchini umezidi kuingia matatani baada ya leo serikali kulifungia gazeti la kila siku la Tanzania Daima kwa siku tisini (90), anaandika Faki Sosi.
Katika kipindi cha takribani mwezi mmoja na siku nne serikali imefunga magazeti matatu yakiwamo ya MwanaHALISI, Raia Mwema na leo Tanzania Daima.
Kati ya Septemba 19 na Oktoba 24 mwaka huu serikali imeyafungia magazeti hayo.
MwanaHALISI lilifungwa kwa kuandika habari iliyokuwa na kichwa cha habari, ”Tumuombee Magufuli au Lissu, Raia
Mwema liliandika habari iliyosomeka Magufuli urais utamshinda na Tanzania Daima juzi liliandika kwamba asilimia 67 ya Watanzania wanatumia dawa za kurefusha maisha za ARVs.
Serikali imelichukulia hatua za kisheria gazeti la Tanzania Daima kwa mwendelezo wa kuandia habari za uongo….Taarifa kamili inakuja. pic.twitter.com/QiVFhJnmQq
— Msemaji Mkuu wa Serikali (@TZMsemajiMkuu) October 24, 2017
Katika habari hiyo ya Tanzania ilionekana kuichukiza serikali na kusababisha Rais John Magufuli kuzungumzia suala hilo alipokuwa akiwatunuku vyeti wajumbe wa kamati za madini Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais alisema habari hiyo ni mbaya kwa taifa kwa sababu inaweza kusababisha wawekezaji wasije kuwekeza nchini kutokana na kuhofia wapi wanaweza kupata wafanyakazi kwa sababu itaonekana Watanzania wengi wanaumwa.
Taarifa ya kuchukuliwa hatua kwa gazeti hilo imechapishwa na Msemaji wa Serikali ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Dk Hassan Abbasi.
Mmoja wa wahariri wa gazeti hilo, Saleh Mohammed amethibitisha kufungiwa gazeti hilo kwa muda wa siku 90.
Leave a comment