Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yafumua mfumo wa Vyuo vya Afya
Afya

Serikali yafumua mfumo wa Vyuo vya Afya

Dk. Zainab Chaula, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya
Spread the love

WIZARA ya Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imefumua mfumo wa uongozi wa vyuo vya afya vidogo, ili kuboresha utoaji wa taaluma nchini. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Hatua hiyo imechukuliwa na Dk. Zainab Chaula, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, katika mkutano wa wakuu wa vyuo vya afya 37, uliofanyika jijini Dodoma.

Dk. Chaula ameunganisha vyuo hivyo, na kupelekea idadi ya vyuo hivyo kupungua, kutoka vyuo 37 hadi kufikia tisa.

 “Wizara imeona ili kuboresha utoaji taaluma katika vyuo vyake,  ni vyema kubadilisha mfumo uliopo wa kuendesha vyuo vidogo vidogo. Na kutengeneza mazingira ya kuwa na vyuo vikubwa vichache, vyenye mfumo mzuri wa kiuongozi,  ili kuzalisha Wataalamu sahihi”, amesema Dk. Chaula.

Dk. Chaula amesema wizara ya afya imechukua hatua ya kufumua uongozi wa vyuo hivyo, baada ya kupokea changamoto mbalimbali, ikiwemo changamoto za uendeshaji wa mafunzo vyuoni uliotokana na uhaba wa watumishi na vifaa vya kufundishia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!