Wednesday , 6 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Mgonjwa wa kwanza wa Corona agundulika Tanzania
AfyaHabari Mchanganyiko

Mgonjwa wa kwanza wa Corona agundulika Tanzania

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeripoti kuwepo mgonjwa mmoja mwenye ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na Virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uwepo wa mgonjwa huyo imetolewa leo tarehe 16 Machi 2020, Waziri Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, wakati akizungumza na wanahabari.

Waziri Ummy amesema mgonjwa huyo ambaye ni raia wa Tanzania, aliingia nchini tarehe 15 Machi 2020, akitokea nchini Ubelgiji kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) .

Amesema mgonjwa huyo mnamo tarehe 3 Machi mwaka huu aliondoka nchini na kwenda katika nchi za Sweden na Denmark alikokuwa kati ya tarege 5 hadi 13 Machi 2020.

“Alipowasili akafanyiwa ukaguzi na kuonekana kutokuwa na homa baadae alianza kujisikia vibaya akiwa hotelini na kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru ambapo sampuli ilipelekwa maabara ya taifa ya afya ya jamii iliyopo Dar es Salaa kwa ajili ya uchunguzi,” amesema Waziri Ummy na kuongeza:

“Vipimo vya maabara vimethibitisha kuwa mtu huyu ana maambukizi ya ugonjwa wa Corona. Mgonjwa anaendelea vizuri na matibabu.”

Waziri Ummy amewataka Watanzania kuchukua hatua juu ya janga hilo kwa kufuata ushauri unaotolewa na mamlaka za afya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

error: Content is protected !!