Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali ya Tanzania yaonya wafanyabiashara ukwepaji kodi
Habari za Siasa

Serikali ya Tanzania yaonya wafanyabiashara ukwepaji kodi

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imetangaza kuanza kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wanaowaongoza wananchi kukwepa kulipa kodi. Anariooti Noela Shila, TUDARCo … (endelea).

Onyo hilo limetolewa leo Ijumaa, tarehe 20 Agosti 2021 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Dk. Mwigulu amesema, hivi karibuni imeibuka tabia ya baadhi ya wafanyabiashara kuwapunguzia bei wananchi wanaokubali kununua bidhaa zao bila kuchukua risiti, ili kujitengenezea mazingira ya kutokatwa kodi.

“Wafanyabiashara waache kuwaongoza Watanzania kukwepa kodi, ili eneo ukifika dukani mtu anakuuliza unataka kulipia hii bidhaa, anakwambia bei yenye risiti ni laki tano, isiyo na risiti laki tatu.”

“Hiki ni kinyume cha sheria, tukatae hawa wanaofundisha wananchi kukwepa kodi na wakiendelea tutawafikisha kwenye mikono ya sheria,” amesema Dk. Mwigulu.

Waziri huyo amewaomba wananchi wasijiingize katika mchezo huo kwa kuwa ni kinyume cha sheria, lakini pia kinaikosesha Serikali fedha za kuwahudumia.

“Penye manunuzi dai upewe risiti na wewe unayetaka kuweka punguzo kukwepa kodi ni uvunjifu wa sheria na sheria tumeweka kodi lazima ilipwe,” amesema Dk. Mwigulu na kuongeza:

“Unataka kuhamasisha asichukue risiti, ukiona hivyo anakufundisha kuvunja sheria kwa kukwepa kodi, usipochukua risiti wakati mwingine anachukua ile hela. Hivyo ile hela ya kuleta madawati na dawa anachukua yeye. Tukiwabani tutawachukulia hatua kali.”

2 Comments

  • Hakuna jipya hapa. Ni ya siku nyingi. Tunataka kuona hatua zikichukuliwa. Fikeni hapo kariakoo na kuona ni maduka mangapi yana mashine za risiti? Chache sana
    Waziri acha kupiga siasa

  • Mikataba ya makampuni makubwa ya uchimbaji madini na makanikia ni ya miaka mingapi?
    Kwa nini watanzania hatuambiwi? Hizi siyo siri….
    Tungeni sheria ya miaka 3 kwanza wakifanya vizuri, miaka inaongezwa kuwa 5. Wakiendelea vizuri 10. Hakuna 20, 30, n.k. Huo ni ujinga unaozuia usimamiaji wa madini yetu. Zungukeni dunia nzima. Tunadanganywa eti mtaji ni mkubwa….huu ni uongo. Uizi ndiyo mkubwa ukiwa na mikataba mirefu unashindwa kumbana au hata kumbadilisha. Huu ni ujinga wetu. Siyo was.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!