Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari Serikali ya Rwanda yashutumiwa kwa kukandamiza uhuru wa kujieleza
HabariKimataifa

Serikali ya Rwanda yashutumiwa kwa kukandamiza uhuru wa kujieleza

Spread the love

MAELFU ya Watu Wamenyanyaswa , kutishwa na kufunguliwa mashitaka kwa kuwa na maoni muhimu kuhusu Serikali ya Rwanda , Humani Raght Watch [HRW] inaeleza

Taarifa hiyo imetolewa makao makuu nchini Marekani leo alhamisi tarehe 17 machi 2022 imetaka kuachiliwa haraka kwa wanaharakati , waandishi wa Habari na Viongozi wa upinzani waliokamatwa nchini Rwanda .

Aidha mnamo mwaka 1994, hotuba za chuki zilitangazwa kwenye vyombo vya Habari , zilichangia kuchochea mauaji ya halaiki ya Rwanda ambayo yaliuwa watu takribani 800,000 ndani ya siku 100

Zaidi ya miaka miwili imepita , Human Right Watch imesema kuwa kukagua hotuba na kuwawekea vikwazo wanahabari , wanaotoa maoni yao Youtube kumepita kiasi .

Hata hivyo ripoti hiyo iliyoangaziwa na nyota wa Youtube anayefahamika kwa jina la Dieudonne Niyonsenga , imetazamwa mara milioni 15 lakini mtayarishaji huyo maudhui alishitakiwa na kutumikia kifungo cha miaka saba jera , kwa kosa la kuwadhalilisha maafisa wa Umma baada ya kuchapisha msururu wa video akiwashutumu Wanajeshi kwa kuwadhulumu watu wanaoishi katika vitongoji duni .

Serikali ya Rwanda inayoongozwa na Rais Paul Kagame haijatoa tamko lolote kuhusiana na ripoti iliyotolewa .

Shirika la Human Right Watch linatumaini ripoti yake italeta mwamko kuhusu ukandamizaji wa uhuru wa kujieleza ulioripotiwa nchi .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!