Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Serikali ya Misri yawatoa kifungoni mashabiki
Michezo

Serikali ya Misri yawatoa kifungoni mashabiki

Spread the love

SERIKLI ya Misri kupitia Waziri wa Michezo, Ashraf Sobhy ametangaza rasmi kuwaruhusu mashabiki wa mpira wa miguu kuingia uwanjani katika michezo ya Ligi Kuu nchini humo toka walipopigwa marufuku mwaka 2012. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mashabiki hao walifungiwa kuingia uwanjani toka 1 Febuari, 2012 baada ya vurugu kubwa kuibuka katika mchezo uliowakutanisha Al Masry dhidi ya Al Ahly kwenye dimba la Port Said nakupelekea mashabiki 74 kufariki dunia na wengine zaidi ya 500 kujeruhiwa.

Wapenzi hao wa soka wataanza kuingia viwanjani kuanzia tarehe 1 septemba, 2018 na kushuhudia michezo tofauti ya ligi kuu lakini waziri huyo alisisitiza watazamaji hawatakiwi kuzidi 500 kwa kila mchezo.

Ligi hiyo ya ambayo ina jumla ya timu 18 ni moja ya ligi bora na yenye ushindani kwa sasa barani Afrika, licha ya kuwa na changamoto ya baadhi ya mashabiki wake kuwa na fujo wawapo viwanjani kwenye michezo ya ndani ya ligi na hata ile ya kimataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!