Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Michezo Serikali ya Misri yawatoa kifungoni mashabiki
Michezo

Serikali ya Misri yawatoa kifungoni mashabiki

Spread the love

SERIKLI ya Misri kupitia Waziri wa Michezo, Ashraf Sobhy ametangaza rasmi kuwaruhusu mashabiki wa mpira wa miguu kuingia uwanjani katika michezo ya Ligi Kuu nchini humo toka walipopigwa marufuku mwaka 2012. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mashabiki hao walifungiwa kuingia uwanjani toka 1 Febuari, 2012 baada ya vurugu kubwa kuibuka katika mchezo uliowakutanisha Al Masry dhidi ya Al Ahly kwenye dimba la Port Said nakupelekea mashabiki 74 kufariki dunia na wengine zaidi ya 500 kujeruhiwa.

Wapenzi hao wa soka wataanza kuingia viwanjani kuanzia tarehe 1 septemba, 2018 na kushuhudia michezo tofauti ya ligi kuu lakini waziri huyo alisisitiza watazamaji hawatakiwi kuzidi 500 kwa kila mchezo.

Ligi hiyo ya ambayo ina jumla ya timu 18 ni moja ya ligi bora na yenye ushindani kwa sasa barani Afrika, licha ya kuwa na changamoto ya baadhi ya mashabiki wake kuwa na fujo wawapo viwanjani kwenye michezo ya ndani ya ligi na hata ile ya kimataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!