Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali ya JPM yawafuta machozi wajane wa Aboud Jumbe
Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya JPM yawafuta machozi wajane wa Aboud Jumbe

Spread the love

SERIKALI ya Rais John Magufuli imewafuta machozi wajane wa aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaji Aboud Mwinyi Jumbe kwa kuwapa gari kwa ajili ya usafi. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Alhaji Aboud Jumbe ameacha wake wawili ambao wamekabidhiwa gari hiyo na George Mkuchika leo hii jijini Dar es Salaam ambapo ni utekelezaji wa Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Viongozi wa Kisiasa Na. 3 ya mwaka 1999 na Marekebisho yake ya mwaka 2005 inayoelekeza utoaji wa stahili kwa wajane wa viongozi wa Kitaifa Wastaafu.

Sambamba na kuenzi mchango Aboud Jumbe, Mkuchika amesema kuwa, kwa mujibu wa sheria hiyo, stahili za wajane kwa viongozi wa Kitaifa Wastaafu ni pamoja na malipo ya pensheni, malipo ya posho ya matunzo ya kila mwezi, gharama za matibabu katika hospitali zilizomo nchini na kupatiwa huduma ya usafiri.

Mkuchika amesema, alikuwa ni kiongozi mahiri, jasiri na mchapakazi aliyeweza kutuliza machafuko yaliyowahi kutokea Zanzibar na amefanya kazi ya kuwaunganisha watanzania.

Ziara Mkuchika ni mwendelezo wa kuwajulia hali viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa lengo la kuboresha huduma wanazopatiwa na Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!