Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali watilia shaka uraia wa Abdul Nondo
Habari za Siasa

Serikali watilia shaka uraia wa Abdul Nondo

Mkurugenzi wa Idara ya Haki na Wajibu wa Wanafunzi Tanzania, Abdul Nondo
Spread the love

MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ameitwa Makao Makuu ya Uhamiaji kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu uraia wake. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Sheria wa TSNP, Paul Kisabo imeeleza kuwa Nondo ametakiwa kwenye ofisi hizo ili kuhojiwa kuhusu uraia wake na ndugu zake.

”Kwa muda wa takribani wiki moja mpaka sasa Nondo amekuwa akihitajika Uhamiaji ili akahojiwe kuhusu taarifa za uraia wake pamoja na za ndugu zake,” imeeleza taarifa hiyo.

Leo Nondo alifika katika ofisi hizo na kuhojiwa baada kutoka kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam alipokwenda kusikiliza kesi yake anayowashataki Mkuu wa Upelelezi, Mwanasheria Mkuu pamja na Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa kuchelewa kumpeleka makahamani.

Mnamo saa sita mchana tuliweza kumfikisha Abdul Nondo Makao Makuu ya ofisi za Uhamiaji mkoa (makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani)
Tulipata kuhoji alichoitiwa na anachotakiwa kujaza katika fomu aliyopatiwa.

”Tuliambiwa wanataka kupata taarifa zake binafsi, za wazazi wake, babu na bibi zake pande zote mbili (upande wa baba na upande wa mama)
pamoja na za ndugu zake, kwani Afisa uhamiaji mkoa alitamka kuwa sheria inawaruhusu kumuhoji mtu yeyote wanaotilia mashaka uraia wake na kuwa wanamashaka na uraia wa Abdul Nondo, hivyo awathibitishie kuwa yeye ni Raia wa Tanzania”

Baada ya hapo afisa uhamiaji aliyekabidhiwa jukumu la kumhoji Abdul Nondo alisema kwamba Apliri 20, 2018 Abdul Nondo anapaswa kupeleka cheti chake cha kuzaliwa, cheti cha kuzaliwa cha baba yake, mama yake, cha bibi na babu mzaa baba na mzaa mama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!