MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ameitwa Makao Makuu ya Uhamiaji kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu uraia wake. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Sheria wa TSNP, Paul Kisabo imeeleza kuwa Nondo ametakiwa kwenye ofisi hizo ili kuhojiwa kuhusu uraia wake na ndugu zake.
”Kwa muda wa takribani wiki moja mpaka sasa Nondo amekuwa akihitajika Uhamiaji ili akahojiwe kuhusu taarifa za uraia wake pamoja na za ndugu zake,” imeeleza taarifa hiyo.
Leo Nondo alifika katika ofisi hizo na kuhojiwa baada kutoka kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam alipokwenda kusikiliza kesi yake anayowashataki Mkuu wa Upelelezi, Mwanasheria Mkuu pamja na Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa kuchelewa kumpeleka makahamani.
Mnamo saa sita mchana tuliweza kumfikisha Abdul Nondo Makao Makuu ya ofisi za Uhamiaji mkoa (makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani)
Tulipata kuhoji alichoitiwa na anachotakiwa kujaza katika fomu aliyopatiwa.
”Tuliambiwa wanataka kupata taarifa zake binafsi, za wazazi wake, babu na bibi zake pande zote mbili (upande wa baba na upande wa mama)
pamoja na za ndugu zake, kwani Afisa uhamiaji mkoa alitamka kuwa sheria inawaruhusu kumuhoji mtu yeyote wanaotilia mashaka uraia wake na kuwa wanamashaka na uraia wa Abdul Nondo, hivyo awathibitishie kuwa yeye ni Raia wa Tanzania”
Baada ya hapo afisa uhamiaji aliyekabidhiwa jukumu la kumhoji Abdul Nondo alisema kwamba Apliri 20, 2018 Abdul Nondo anapaswa kupeleka cheti chake cha kuzaliwa, cheti cha kuzaliwa cha baba yake, mama yake, cha bibi na babu mzaa baba na mzaa mama.
Leave a comment