Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Serikali, TLS kukaa meza moja
Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali, TLS kukaa meza moja

Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria
Spread the love

 

Serikali ya Tanzania imewaita mezani viongozi wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), kwa ajili ya kujadili namna ya kuimarisha mahusiano ya pande zote mbili. Anaripoti Hamis Mguta, Arusha … (endelea).

Wito huo umetolewa leo Alhamisi tarehe 14 Aprili 2021, na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju wakati akifungua Mkutano Mkuu wa TLS unaofanyika jijini Arusha.

Mpanju ameutaka uongozi mpya wa TLS utakaochaguliwa kesho Ijuma tarehe 16 Aprili 2021, kukaa meza moja na Serikali kujadili changamoto zilizopo ikiwepo baadhi ya vifungu vya sheria vinavyodaiwa kuwa kandamizi kwa tasnia hiyo.

“Niombe uongozi unaokuja tuwe na nia njema, tutizame mabadiliko ya sheria yaliyopo kama yataleta ufanisi na kama haitaketa ufanisi serikali iko tutakaa mezani tuangalie. Lakini tusianze kupinga mwanzo.

“Ni wakati uongozi mpya kukaa kutengeneza hoja na  kwenda mezani. Haileti tija kusimama hapa kutoa tamko bila kushauriana na wanaohusika sote tuanjenga nyumba moja,” amesema Mpanju.

 

 

Mpanju ametoa kauli hiyo baada ya Rais wa TLS anayemaliza muda wake, Dk. Lugemeleza Nshala, kusema mabadiliko ya Sheria inayoongoza chama hicho, yaliyofanyika mwaka jana, yanababa uhuru wa chama hicho na mawakili kutekeleza majukumu yao.

Sambamba na hilo, Mpanju amewaasa viongozi wa TLS kutojihusisha na masuala ya siasa na uanaharakati.

“Haina masilahi wala tija kujiingiza kwenye uanaharakati na kuacha jukumu la msingi la kitaaluma. Haina haja wa tija kujiingiza kwenye siasa. Nawasihi viongozi watakaokuja nenda kwenye msingi wa malengo ya serikali ya kukuza chama na taaluma ya Sheria,” amesema Mpanju.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!