Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali: Mwaka 2015 – 19 tumeajiri watu 184,141
Habari za Siasa

Serikali: Mwaka 2015 – 19 tumeajiri watu 184,141

Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira.
Spread the love

SERIKALI imesema, imeajiri watu 184141, kuanzia mwaka 2015 hadi 2019. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Takwimu hizo zimetolewa leo tarehe 5 Novemba 2019, bungeni jijini Dodoma na Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira.

Wakati huo huo, Mavunde amesema miradi ya maendeleo imetoa ajira  787405, na sekta binafsi imeajiri watu 646,466.

“Kuanzia mwaka 2015 hadi 2019 serikali kupitia taasisi zake imeajiri 184,141, ajira zilizotolewa kupitia miradi ya maendeleo ya serikali ni 787405, na ajira  646,466 zilitolewa na sekta binafsi,” amesema Mavunde.

Mavunde ametoa takwimu hizo wakati akijibu swali la Anna Gidarya, Mbunge Viti Maalumu mkoani Manyara.

Mavunde ametoa takwimu hizo wakati akijibu swali la Anna Gidarya, Mbunge Viti Maalumu mkoani Manyara, aliyehoji mkakati wa serikali katika kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana wanaohitimu vyuo vikuu.

Gidarya amesema, kuna kundi kubwa la vijana halina ajira kwa zaidi ya miaka mitatu, na kudai kwamba serikali imekuwa kimya katika kutoa majibu kuhusu changamoto hiyo.

Lakini, swali hilo limejibiwa na Mavunde, aliyesema kwamba serikali inaendelea kuajiri watu kupitia taasisi zake kila mwaka, kwa kuzingatia mahitaji na bajeti. Pia, miradi ya maendeleo pamoja na ongezeko la shughuli za kiuchumi, imeongeza wigo wa utoaji ajira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!