Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali: Mradi wa REA haulipi fidia
Habari Mchanganyiko

Serikali: Mradi wa REA haulipi fidia

Spread the love

SERIKALI imesema, hakuna malipo ya fidia kwenye maeneo ya wananchi,yanayopitiwa na mradi wa usambazaji umeme vijijini unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Anaripoti Regina Mkonde …(endeea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 10 Juni 2019 bungeni jijini Dodoma na Subira Mgalu, Naibu Waziri wa Nishati wakati akijibu swali la Mbunge Viti Maalum mkoani Arusha, Catherine Magige.

Swali la Magige lilihoji kwamba, lini serikali itakamilisha mchakato wa ulipaji fidia kwa wananchi zaidi ya 2,000 wa Wilaya ya Longido na Monduli mkoani Arusha, ambao maeneo yao yalipitiwa na mradi wa REA.

Akijibu swali hili, Mgalu amesema miradi ya umeme vijijini haina fidia, kwa kuwa serikali imempunguzia mwananchi mzigo wa gharama za kuunganishiwa nishati ya umeme kwa kugharamia kwa asilimia mia fedha za ujenzi wa miundombinu pamoja na huduma za kuunganishiwa umeme.

Amesema ili kuhakikisha kwamba adhma ya serikali ya kuunganishia umeme wanawancho wote hasa wa vijijini, ni vyema wananchi wakatoa ushirikiano katika miradi hiyo ikiwemo kutodai fidia.

“Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inatekeleza mradi huu,  lengo ni kuhakikisha Watanzania zaidi ya asilimia 85 wanatum ia umeme ifikapo 2025. Ili kuhakikisha lengo hili linafikiwa, serikali inagharamia gharama za ujenzi wa miundombinu na gharama ya kufikisha umeme  kwa asilimia 100 na wananchi kulipa sh. 27000 tu ikiwa ni kodi ya VAT,” amesema Mgalu na kuongeza.

“Hivyo miradi ya umeme vijijini haina fidia, natumia fursa hii kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano katika miradi huu ikiwemo kutodai fidia. Sisi tunaendelea kuelimisha kadri tunapopata fursa, tunawaomba watupe nafasi zaidi.”

Aidha, Mgalu amesema serikali itahakikisha vijiji vilivyopitiwa na msongo mkubwa wa umeme ambavyo havijaunganishiwa umeme, vyote vitaunganishwa na huduma hiyo ifikapo mwezi Desemba 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!