Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kuvuna 50 kwa 50 kwenye dhahabu
Habari za Siasa

Serikali kuvuna 50 kwa 50 kwenye dhahabu

Spread the love

HATIMAYE mazungumzo kati ya Tanzania na Kampuni ya Barrick Gold kuhusu sekta ya madini yaliyodumu kwa takribani miezi mitano yamehimitishwa jijini Dar es Salaam, anaandika Faki Sosi.

Rais John Magufuli leo amepokea ripoti ya makubaliano hayo ambayo yalihusisha watalaam 25 kutoka kampuni ya Barrick na wawakilishi wanane wa Tanzania wakiongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi.

Moja ya makubaliano yaliyofikiwa ni pamoja na Tanzania kugawana faida 50 kwa 50 na kampuni ya Barrick Gold .

Aidha, katika makubaliano hayo Barrick wamekubali kulipa fedha mbalimbali kwa Halmashauri wanapochimba dhahabu.

Kupitia makubaliano hayo, kampuni hiyo imekubali kupanua wigo wa ajira kwa Watanzania pamoja na kujenga maabara na kiwanda cha kuchakata makanikia hapa nchini.

Profesa Kabudi amesema kampuni ya Barrick, wamekubali masharti yote yaliyoko kwenye sheria mpya ya madini na kukubali kuingia ubia wa asilimia 50 kwa 50 kwenye biashara ya madini.

Kwa upande wake, mwenyekiti mtendaji wa kampuni ya Barrick Gold Profesa . John Thornton alimpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi wa kutaka muafaka juu ya makanikia.

“Tumekubaliana kulipa dola za Marekani milioni 300 sawa na Sh. bilioni 700 kama sehemu ya kujenga uaminifu na kuendeleza biashara,” amesema

Rais Magufili amesema baada ya kukamilika mazungumzo haya sasa watalaam wa Tanzania waanze kujadiliana katika sekta ya Almasi na Tanzanite.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!