WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itapunguza kodi ya sukari itakayoingizwa nchini kwa hadi asilimia 10 ili kupata unafuu wa bei ya didhaa hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Dk. Mwiguli ameyasema hayo leo Jumatano tarehe 11 Aprili wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa bei nchini.
Amesema mbali na sukari pia wataangalia tozo za Serikali katika nishati ya mafuta ambazo zinaweza kupunguzwa na kazi hiyo itachukua hadi wiki moja kukamilisha.
Pia amesema watakwenda kuangalia kodi katika mafuta ya kula ambapo amesema wameshailekeza Mamlaka ya Mapato Tanzania kuangalia ndani ya mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu kuweka viwango vipya vya kodi ili kupunguza makali.
“Tutashirikiana na wenzetu wa sekta binafsi ili kuangalia kiwango ambacho kitasaidia wananchi waweze kupumua kwa kupata unafuu wa bei,”
“Kwa maana hiyo tutakuwa tumeshagusa sukari, nishati ya mafuta, mafuta ya kula na kwenye mbolea kama ambavyo Waziri (Dk. Kijaji) ameeleza,” amesema Nchemba.
Vilevile amesema watapunguza sehemu ya gharama zilizokuwa zinaongezeka kwenye usafiri kwa kupunguza gharama kwenye vifaa vya usairishaji ikiwemo semi trela n.k.
Leave a comment