Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Biashara Serikali kupunguza kodi kwenye sukari, mafuta
Biashara

Serikali kupunguza kodi kwenye sukari, mafuta

Spread the love

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itapunguza kodi ya sukari itakayoingizwa nchini kwa hadi asilimia 10 ili kupata unafuu wa bei ya didhaa hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Dk. Mwiguli ameyasema hayo leo Jumatano tarehe 11 Aprili wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa bei nchini.

Amesema mbali na sukari pia wataangalia tozo za Serikali katika nishati ya mafuta ambazo zinaweza kupunguzwa na kazi hiyo itachukua hadi wiki moja kukamilisha.

Pia amesema watakwenda kuangalia kodi katika mafuta ya kula ambapo amesema wameshailekeza Mamlaka ya Mapato Tanzania kuangalia ndani ya mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu kuweka viwango vipya vya kodi ili kupunguza makali.

“Tutashirikiana na wenzetu wa sekta binafsi ili kuangalia kiwango ambacho kitasaidia wananchi waweze kupumua kwa kupata unafuu wa bei,”

“Kwa maana hiyo tutakuwa tumeshagusa sukari, nishati ya mafuta, mafuta ya kula na kwenye mbolea kama ambavyo Waziri (Dk. Kijaji) ameeleza,” amesema Nchemba.

Vilevile amesema watapunguza sehemu ya gharama zilizokuwa zinaongezeka kwenye usafiri kwa kupunguza gharama kwenye vifaa vya usairishaji ikiwemo semi trela n.k.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Biashara

Meridianbet yatoa msaada Makongo

Spread the love  MABINGWA wa michezo ya kubashiri kampuni ya Meridianbet imefika...

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Biashara

Shinda mpaka 1,250,000/= ukicheza shindano la Expanse Kasino

Spread the love  KUBWA zaidi kutoka Meridianbet ni promosheni ya Expanse ambayo...

error: Content is protected !!