Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kumuongezea nguvu CAG ufuatiliaji miradi
Habari za Siasa

Serikali kumuongezea nguvu CAG ufuatiliaji miradi

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesema itaongeza fedha katika Ofisi ya mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ili kuiwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ikiwemo kuhakikisha miradi mikubwa inatekelezwa kulingana na thamani ya fedha inayotumika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni jijini Dodoma, wakati anawasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa 2022/23, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema ongezeko hilo litasaidia ofisi ya CAG kuwa na watumishi wa kutosha kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa miradi hiyo.

“Napendekeza kumwongezea fedha CAG ili apate watumishi wa kutosha kwa kuajiri na kuwahamisha watumishi kutoka idara yoyote ya Serikali na kuwajengea uwezo kwa mafunzo na weledi wa ukaguzi wa thamani ya fedha ili kuweza kukabiliana na tatizo hili,” amesema Dk. Mwigulu.

Katika hatua nyingine, Dk. Mwigulu amesema Serikali itaendelea kuimarisha vitengo vya ukaguzi wa ndani kwa kuvijengea uwezo wa kitaaluma na kuongeza idadi ya watumishi katika fani mbalimbali kama TEHAMA, uhandisi, ukadiriaji majenzi, wakemia na wanasheria.

“Ili kuondokana na dhana ya wakaguzi wa ndani kuwa na taaluma ya fedha pekee. Aidha, Serikali itafanya marekebisho ya Kanuni za Fedha za Umma kwa kuziwezesha Kamati za Ukaguzi kuwa na wajumbe wa nje watatu ikiwemo Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi ili kuongeza uhuru na ufanisi wa kamati za ukaguzi kupitia Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2022,” amesema Dk. Mwigulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!