Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali kuja na masharti mapya usajili maduka ya fedha za kigeni
Habari Mchanganyiko

Serikali kuja na masharti mapya usajili maduka ya fedha za kigeni

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, inatarajia kutangaza masharti mapya ya usajili wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni, ili kuchochea ukuaji wa biashara hiyo nchini. Anariupoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 24 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Hamad Chande, akimjibu Mbunge wa Kinondoni, Abbas Tarimba, aliyehoji mkakati wa Serikali katika kupanua biashara ya ubadilishaji fedha za kigeni ili kuboresha huduma hiyo kwa raia wa kigeni hasa watalii.

Chande amesema, kwa sasa watalaamu wa Wizara ya Fedha na Mipango, wako katika hatua za mwisho za kuchakata masharti hayo na kwamba hivi karibuni yatatangazwa, huku akiahidi kwamba yatakuwa nafuu.

“Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa aliyofanya kutangaza utalii na vivutio vyetu ndani ya nchi yetu. Serikali tumezingatia suala lako la kupunguza masharti, wataalamu wamekaa na wanachakata. Hivi karibuni yatatoka masharti nafuu sana kwa ajili ya wawekezaji wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni,” amesema Chande.

Katika hatua nyingine, Chande amejibu swali la Tarimba lililohoji lini Serikali itaondoa changamoto ya tofauti ya gharama za kubadilisha fedha za kigeni hasa Dola za Marekani, akisema Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (B.o.T), itatoa bei elekezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!