Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali kufanya utafiti wa hali ya umasikini
Habari Mchanganyiko

Serikali kufanya utafiti wa hali ya umasikini

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania ipo katika maandalizi ya mwisho ya kufanya utafiti wa hali ya umasikini nchini kwa mwaka 2023/2024. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumatano, tarehe 18 Januari 2023 na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dk. Albina Chuwa, katika kikao kazi cha kujadili hali ya mfumuko wa bei.

“Tunategemea kufanya utafiti kwenye mapato na matumizi ya kaya ambayo itatupa hali ya umasikini, tunafanya maandalizi ya mwisho ya kufanya utafiti,” amesema Dk. Chuwa.

Mtakwimu huyo wa Serikali amesema utafiti wa mwisho wa hali ya umasikini ulifanyika 2017/18, ambapo ulionyesha asilimia 28.2 ya wananchi wanaishi chini ya mstari wa umasikini.

Kuhusu Pato la Taifa (GDP), Dk. Chuwa amesema maoteo ya ukuaji wake ni asilimia 5.3, kutokana na majanga yanayoendelea kutokea duniani, hususan athari za vita kati ya Urusi na Ukraine.

“Maoteo tuliyofanya yalituonyesha GDP itakuwa kwa asilimia 5.3 katika robo ya mwaka, lakini tuna sera ya kufanya marejeo kulingana na global crisis ambapo tumepata maoteo ya asilimia 5.2 lakini Machi 2023 tutajua kama tumebaki kwenye maoteo yaleyale,” amesema Dk. Chuwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!