SERIKALI ya Tanzania ipo katika maandalizi ya mwisho ya kufanya utafiti wa hali ya umasikini nchini kwa mwaka 2023/2024. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Hayo yamesemwa leo Jumatano, tarehe 18 Januari 2023 na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dk. Albina Chuwa, katika kikao kazi cha kujadili hali ya mfumuko wa bei.
“Tunategemea kufanya utafiti kwenye mapato na matumizi ya kaya ambayo itatupa hali ya umasikini, tunafanya maandalizi ya mwisho ya kufanya utafiti,” amesema Dk. Chuwa.
Mtakwimu huyo wa Serikali amesema utafiti wa mwisho wa hali ya umasikini ulifanyika 2017/18, ambapo ulionyesha asilimia 28.2 ya wananchi wanaishi chini ya mstari wa umasikini.
Kuhusu Pato la Taifa (GDP), Dk. Chuwa amesema maoteo ya ukuaji wake ni asilimia 5.3, kutokana na majanga yanayoendelea kutokea duniani, hususan athari za vita kati ya Urusi na Ukraine.
“Maoteo tuliyofanya yalituonyesha GDP itakuwa kwa asilimia 5.3 katika robo ya mwaka, lakini tuna sera ya kufanya marejeo kulingana na global crisis ambapo tumepata maoteo ya asilimia 5.2 lakini Machi 2023 tutajua kama tumebaki kwenye maoteo yaleyale,” amesema Dk. Chuwa.
Leave a comment