Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Serikali kuanzisha mradi umaliziaji maboma yaliyoanzishwa na wananchi
HabariHabari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi umaliziaji maboma yaliyoanzishwa na wananchi

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake kupitia Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, itaandaa mradi wa kumalizia maboma yaliyoanza kujengwa na wananchi, ikiwemo ya madarasa na zahanati. Anaripoti Bupe Mwakiteleko, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 18 Mei 2022, katika halfa ya uzinduzi wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda, iliyofanyika mkoani Tabora na kurushwa mbashara katika vyombo vya habari.

Kiongozi huyo wa Tanzania, ametoa ahadi hiyo baada ya uongozi wa Mkoa wa Tabora, kuiomba Serikali yake imalizie maboma takribani 120 ya madarasa, yaliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi na kuishia kati.

“Bajeti ya TAMISEMI kwa kiwango kikubwa itaenda kukamilisha maboma haya ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi. Lakini pia tunajitahidi kuwa na mradi kupitia TAMISEMI, kwenda kumalizia maboma ya zahanati ambayo tayari wananchi wameonesha nguvu zao,”amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!