Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Serikali imesema haina takwimu utekaji watoto
Habari Mchanganyiko

Serikali imesema haina takwimu utekaji watoto

Dk.Hamisi Kigwangalla, waziri wa Maliasili na Utalii
Spread the love

SERIKALI imesema kuwa haina takwimu za watoto waliokeketwa nchini kwa kuwa vitendo vya ukeketaji kufanyika kwa siri, anaandika Dany Tibason.

Mbali na kutokuwa na takwimu sahihi za watoto waliokeketwa pia serikali imesema kuwa haina takwimu ya watuhumiwa wa vitendo hivyo ambao mpaka sasa wamepelekwa mahakamani mpaka sasa.

Kauli hiyo imetolewa na bungeni leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk Khamisi Kigwangwala alipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalum, Anna Gidarya (Chadema).

Mbunge huyo akiuliza swali la nyongeza, alitaka kujua kama serikali ina takwimu za watoto waliokeketwa pamoja na kutaka kujua kama serikali ina takwimu za watu waliopelekwa mahakamani kutokana na vitendo vya ukeketeaji.

Awali katika swali la msingi la ambunge huyo alitaka kujua serikali ina mpango gani wa kukabiliana na ukatili ambao wanafanyiwa watoto wa kike kwa kukeketwa.

“Mkoa wa Manyara ni mojawapo ya mikoa inayoongoza kwa ukeketaji wa watoto wa kike takwimu za mwaka 2017 zinaonesha kuwa mkoa huo unaongoza kitaifa.

“Je serikali ina mpango mathubuti wa kukomesha ukatili huu wa kijinsia pamoja na kutoa semina elekezi kuhusu madhara yanayotokana na ukeketaji wa watoto wa kike hususani wilaya ya Hanang’, Simanjiro, Kiteto na Mbulu.

“Ngariba sasa wanatumia njia mbadala za kuwakeketa watoto wa kike wa kuanzia miezi sita hadi mwaka mmoja na miezi sita, je serikali ina mkakati gani wa kuwakamata ngariba,wote wanaofanya ukatili huo kwa kuwachukulia hatua ili wawe sehemu ya fundisho ili kukomesha ukatili huo” alihoji Mbunge.

Akijibu maswali hayo Dk. Kigwangwala alisema vitendo vya ukeketaji vinafanywa kwa siri zaidi hivyo serikali haina takwimu za watoto waliokeketwa wala waliopelekwa mahakamani.

Hata hivyo, alisema kuwa serikali inatoa makatazo ya kuwakeketa watoto wa kike kwani kwa kufanya hivyo ni kuwanyanyasa kijinsia watoto wa kike.

Amesema kwa sasa serikali inatoa elimu kwa ngariba wote katika mikoa ambayo bado inaendelea kukeketa watoto wa kike ikiwamo kuwaeleza madhara ukeketaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!