Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Serengeti Girls yatinga bungeni, Nahodha ahutubia
Michezo

Serengeti Girls yatinga bungeni, Nahodha ahutubia

Spread the love

 

NI heshima kubwa. Ndivyo unaweza kuelezea kile ambacho Timu ya Taifa ya soka la Wanawake chini ya miaka 17 ‘Serengeti Girls’ ya Tanzania imekipata kwa Bunge la Taifa hilo kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Timu hiyo ya benchi la ufundi na viongozi wa wizara ya utamaduni, sanaa na michezo na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) leo Jumanne, tarehe 7 Juni 2022 wamepewa heshima hiyo na muhimili huo nyeti nchini humo.

Hiyo ni kutokana na mafanikio waliyoyapata ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia nchini India Oktoba 2022 kwa kuwaondoa Cameroon kwa jumla ya magoli 5-1.

Kabla ya timu hiyo kuingia bungeni, kanuni za Bunge zilitenguliwa ili kuruhusu kuingia ukumbini na kupata fursa ya kukaa viti vya wabunge na nahodha wa timu hiyo kulihutubia Bunge hilo.

Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amewapongeza na kuwataka kwenda kuiwakilisha vyema nchi na kuhakikisha wanarudi na Kombe la Dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!