Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Serengeti Boys yafuzu fainali za Vijana
Michezo

Serengeti Boys yafuzu fainali za Vijana

Kikosi cha timu ya Taifa ya vijana chini umri wa miaka 17, Serengeti Boys
Spread the love

HATIMAYE timu ya Taifa ya vijana chini umri wa miaka 17, Serengeti Boys imefuzu kucheza michuano ya kombe la mataifa Afrika baada ya kushinda rufaa walioiweka dhidi ya mchezaji wa timu ya taifa ya Jamuhuri ya Congo, Langa Lesse Bercy kutokana na umri wake.

Congo hapo awali ilifuzu michuano hiyo baada ya kuitoa timu ya Serengeti Boys kwa kuifunga bao moja kwa bila katika mchezo wa marudiano uliofanyika Kinshasa, licha ya Tanzania kushinda mabao 2-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika jijini Dar es salaam.

Kamati ya utendaji ya CAF iliyokaa mjini Libreville, nchini Gabon imeipa ushindi Tanzania, baada ya timu ya Jamhuri ya Congo kumchezesha mchezaji Langa Lesse Bercy aliyezidi umri kinyume na kanuni za michuano hiyo.

Katika kipindi cha nyakati tofauti, CAF walitoa agizo la kwa shirikisho la soka la Jamhuri ya Congo (FECOFOOT) kumpeleka kijana huyo Cairo, Misri kwa ajiri ya vipimo vya MRI iliwaweze kujilidhisha juu ya tuhuma hizo lakini Congo hawakulifanya hilo

Fainali hizo zinatarajia kufanyika Aprili 2, mwaka huu katika nchi ya Gabon, ambao wameandaa fainali za kombe la mataifa Afrika mwaka huu, baada ya CAF kuiengua Madagascar kuandaa fainali hizo kutokana kutojilidhisha namna ya maandalizi yalivyokuwa yanafanyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!