Tuesday , 3 October 2023
Kimataifa

Senegal mambo magumu

Spread the love

 

HALI ya wasiwasi nchini Senegal, imezidi kutanda baada ya Ousmane Sonko (46), kiongozi wa upinzani kutuhumiwa kubaka. Mtandao wa Aljazeera unaripoti … (endelea).

Serikali ya nchi hiyo, ilimkamata Sonko Jumatano wiki iliyopita, bila kueleza sababu jambo lililosababisha kuibuka kwa maandamano.

Hata hivyo, kiongozi huyo alifikishwa mahakamani Jumatatu wiki hii ambapo pamoja na makosa mengine, ameyotuhumiwa kubaka.

Wafuasi wa kiongozi huyo wengi wao wakiwa vijana, wameghadhibika na hatua ya Sonko kutuhumiwa ubakaji ambapo wameeleza “ni hila za serikali (ya nchi hiyo) ili kumzima.”

Maandamano makubwa yametikisa mji mkuu wa nchi hiyo, Dakar Jumatatu na kuendelea mpaka sasa. Maduka na huduma zingine zimefungwa ‘kupisha’ rapsha hiyo.

Polisi wa Senegal wamekuwa wakitumia nguvu ikiwemo maji ya washa na mabomu ya machozi kukabili maelfu ya waandamanaji hao.

“Hatuwezi kuruhusu Macky Sall (rais) akakandamiza demokrasia na kumfunga mpinzani wake,” Rama Diop (30), amenukuliwa na Aljazeera akiongeza “Ousmane Sonko anawakilisha matumaini ya maisha bora Senegal.”

Watu watano wanaripotiwa kupoteza maisha kwenye maandamano hayo, tangu yalipoanza Jumatano wiki iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Urusi yafungua milango kwa nchi za Afrika

Spread the loveSERIKALI ya Urusi imefungua milango ya ushirikiano wa kiuchumi, kijamii...

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Putin aita vikundi vya kujitolea vita ya Ukraine

Spread the loveRAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amefungua milango ya ushirikiano kwa...

Kimataifa

Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume

Spread the loveWATU takribani 50 wamefariki dunia huku wengine 50 wakijeruhiwa katika...

error: Content is protected !!