Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko SBL yazindua mfumo wa kufanya mauzo kiganjani kwa wasambazaji wake
Habari Mchanganyiko

SBL yazindua mfumo wa kufanya mauzo kiganjani kwa wasambazaji wake

Spread the love

 

KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL) imezindua mfumo wa aina yake wa kufanya mauzo wenye lengo la kurahisisha na kuongeza ufanisi wa mauzo yake kwa kuwapa wasambazaji wao (Stockists, Wholesalers & Bars) taarifa za kisasa kwa kutumia simu. Hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za SBL kukumbatia maendeleo katika uendeshaji wake na mtindo wa biashara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Programu iliyopewa jina la DIAGEO ONE itakuwa suluhu moja kwa wateja wa SBL na kuwezesha mageuzi ya kiwango cha kimataifa jinsi SBL inavyofanya biashara na wateja wao. SBL ilizindua mfumo huo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam kwa wateja wake muhimu baada ya awamu ya majaribio iliyoanza Februari mwaka huu kumalizika kwa ufanisi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Meneja Mawasiliano na Uendelevu wa SBL, Rispa Hatibu alisema, “SBL tumedhamiria kufanya mageuzi katika shughuli zetu za biashara, hii ni pamoja na kutumia teknolojia na ubunifu ili kuhakikisha kuwa kuna ufanisi katika namna tunavyofanya biashara. SBL ina nafasi kubwa katika sekta hii, na ndio maana tunasimamia ubunifu wa programu kama hizi.”

Aliongeza, “kiwango cha kazi iliyohusika katika kufanikisha jambo hili imekuwa muhimu kwa timu mbali mbali za SBL, EABL, na usaidizi mpana wa kampuni mama ya SBL ili kuhakikisha tunatekeleza kwa ufanisi programu hii mpya ambayo itabadilisha njia za kufanya kazi kwa wateja wetu”

Mkurugenzi wa Mauzo wa kampuni ya Bia ya Serengeti, Christppher Gitau akizungumza katika uzinduzi wa mfumo wa mauzo kiganjani ujulikanao kama Diageo One

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mabadiliko ya Kidijitali wa SBL Chelu Mapolu alisema uzinduzi wa DIAGEO ONE kwa mkoa wa Dar es Salaam unafuatia mafanikio ya awamu ya majaribio ya mfumo huo, ambapo SBL imepima utendaji kazi na ufanisi wa mfumo huo kwa wasambazaji na wateja mbalimbali jijini Dar es Salaam,” tumeifanyia majaribio na tunafurahia kuwaambia wasambazaji na wateja wetu kwamba mfumo huu utaleta mapinduzi makubwa kwa namna SBL inavyofanya mauzo. Kwa mfumo huu wa mauzo, wateja wetu watakuwa na taarifa muhimu zote kiganjani. Mfumo wa Diageo One ni rafiki kwa watumiaji na unafanya mchakato wetu wa uuzaji kuwa rahisi, mzuri na wa kufurahisha zaidi.”

Alibainisha kuwa, baada ya uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, matumizi ya mfumo wa DIAGEO ONE mchongo kiganjani utaanza kutumika kwa awamu nchini kote kwa wasambazaji wote wa bidhaa za SBL kuanzia mwezi Juni ambapo wateja wetu wote watapatiwa mafunzo ya jinsi ya kutumia mfumo huo na njia bora wanayoweza kuutumia ili kurahisisha mchakato wao wa kuagiza na kufanya manunuzi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!