Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Saudi Arabia imekiri kushindwa’
Kimataifa

‘Saudi Arabia imekiri kushindwa’

Adel al-Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia
Spread the love

NAIBU Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassim amesema kuwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia inaonesha kukiri kushindwa kwake baada ya kukubali kuanzishwa maeneo ya kupunguza mivutano nchini Syria, anaandika Jovina Patrick.

Jumapili ya jana Adel al-Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudia akizungumza na waandishi wa habari nchini humo ikiwa ni miaka sita ya vita na baada ya kushindwa makundi ya kigaidi kwa ajili ya kuiondoa madarakani serikali ya Damascus, alisema kuwa Saudia inakubaliana na pendekezo la kuanzishwa maeneo ya kupunguza mizozo nchini humo.

Lengo kuu la mazungumzo hayo ni kutiwa saini makubaliano yenye lengo la kuanzishwa maeneo ya kupunguza migogoro nchini Syria. Kufuatia hali hiyo Sheikh Naim Qassim akizungumza na kanali ya televisheni ya al-Manar amesema kuwa, Saudia inapitia wakati na kipindi kigumu kutokana na kushindwa mipango yake yote katika eneo la Mashariki ya Kati.

Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, muqawama nchini Syria umekuwa ukisajili ushindi na kwamba ushindi huo utaendelea

Ameongeza kuwa, kukombolewa mji wa Aleppo kumefelisha njama za maadui za kutaka kuigawa vipande nchi ya Syria na kwamba kukombolewa mji wa Deir ez-Zor, ni ushindi mwingine mkubwa dhidi ya genge la kigaidi la Daesh.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!