RAIS wa Tanzania amemteua Sauda Kassim Msemo kuwa Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kabla ya uteuzi huo uliofanywa jana Jumatano, tarehe 25 Mei 2022, alikuwa Kamishna wa Fedha za Nje, Wizara ya Fedha na Mipango.
Sauda anakuwa mwanamke wa pili kushika wadhifa ndani ya BoT tangu kuanzishwa kwake, akitanguliwa na Dk. Natu Mwamba aliyekuwa Naibu Gavana kati ya Juni 2011 hadi Juni 2017 enzi za utawala wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Sauda anachukua nafasi ya Dk. Bernad Kibesse aliyekuwa kwenye nafasi hiyo kuanzia Mei 2017 ambaye sasa ameteuliwa na Rais Samia kuwa Balozi.
Leave a comment