Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sasa naomboleza kifo cha mama – kabendera
Habari Mchanganyiko

Sasa naomboleza kifo cha mama – kabendera

Spread the love

ERICK Kabendera, mwandishi wa habari za uchunguzi ndani na nje ya nchi, amesema ‘sasa naomboleza kifo cha mama yangu.” Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Kabendera ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kuachwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, tangu tarehe 5 Agosti 2019 alipokuwa akishikiliwa kwa makosa ya matatu likiwemo la utakatishaji fedha.

Mama yake Kabendera, Verdiana Mjwahuzi alifariki dunia tarehe 31 Desemba 2019 na kuzikwa tarehe 4 Januari 2020, mkoani Kagera.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 24 Agosti 2020, baada kuachiwa huru kwa kulipa faini ya Sh. 250,000 na Sh. 100 milioni baada ya kuamriwa na mahakama, Kabendera amesema atakutana na watu wachache walimfariji tangu akumbane na mkasa huo.

Pia amewashukuru wanahabari wenzake wanaharakati, watu wa kada mbalimbali na Watanzania wote kwa kuwa naye karibu wakati akiwa kwenye matatizo.

Kabendera ameondoka na ndugu zake kwenye viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi saa 10 alasiri.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!