Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Samia: Walioiba pembejeo ruzuku nataka wazione rangi zangu
Habari

Samia: Walioiba pembejeo ruzuku nataka wazione rangi zangu

Spread the love

RAIS SamiaSuluhu Hassan ameiagiza Taasisi yaKuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) “kuwashughulikia kisawasawa” wezi wa pembejeo za ruzuku na fedha za vyama vya ushirika waliokamatwa mkoani Simiyu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Ametoa maagizo hayo leo Jumatatu tarehe 4 Aprili 2022 jijini Dodoma wakati akizindua ugawaji wa vitendea kazi kwa maafisa ugani wa kilimo.

“Wakuu wa mikoa nimeona kwenye habari Mkuu wa Mkoa Simiyu amekamata watu wanaoiba pembejeo za kilimo za ruzuku na hili liko TAKUKURU naomba wazisome zile rangi zangi, nataka washughulikie kisawasawa ili iwe fundishokwa wengine wasiibe na waziri mkuu usimamie hilo,” amesema Rais Samia.

Amesema mwaka jana alielekeza kufanya majaribio ya kutoa ruzuku za pembejeo kwa wakulima na yameonesha mafanikio makubwa.

“Tumepata matokeo mazuri kwenye pamba, nimeelekeza sasa kuwe na mfuko maalum wa pembejeo. Mwaka jana tulitumia Sh 56 Bilioni kwenye pamba, Sh. 61 bilioni kwenye korosho na Sh 32 bilioni kwenye tumbaku. Matokeo kiwanda cha tumbaku Morogoro tunakifungua kwasababu tumbaku imeongezeka.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!