Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Tone moja la maji ni Sh 3,000
Habari za Siasa

Samia: Tone moja la maji ni Sh 3,000

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema maji yangeuzwa kwa kuangalia gharama za miradi tone moja la maji lingeuzwa kwa Sh 3,000. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Badala yake Mkuu huyo wa nchi amesema Serikali inawekeza fedha nyinge kwenye miradi ya maji ili wananchi wafaidike na huduma hiyo.

Ameyasema hayo leo Ijumaa ttarehe 5 Agosti, 2022, wakati akizungumza na wananchi wa Mbalizi mara baada ya kuzindua mradi wa maji wa Shongo-Mbalizi uliogharimu Sh 3.3 bilioni.

Amesema kutokana na gharama kubwa za miradi ndiyo sababu ya sekta binafsi kutowekeza katika miradi ya maji na badala yake Serikali ndiyo inatoa huduma hiyo.

Akifafanua zaidi amesema hivi sasa wannchi watannua uniti mopja yam aji ambayo ni sawa na ndoo 50 za lita 20 kwa Sh 1,100 tofauti na awali ambapo walikuwa wakiuziwa ndoo moja kwa Sh 500.

“Kutokana na gharama za miradi ya maji tone moja la maji lingeuzwa kwa Sh 3,000, tone moja sio hata lita moja. Lakini hapa ndoo 50 za lita 20 tunauziwa Sh 1100, wakati mkinunua maji mlikua mnanunua dumu moja Sh 500…sasa hiyo ndo kazi ya Serikali kuweka fedha wananchi wake wafaidike ndo maana sekta binafsi haipo kwenye maji,” amesema Samia.

Mradi wa maji wa Shongo-Mbalizi uliopo mkoani Mbeya umegharimu Sh3.345 bilioni na utazalisha lita milioni 8-12 za maji kwa siku ukihudumia wakazi 80,000 wa eneo la Mbalizi.

Mradi huo wenye mtandao wa mabomba wa kilomita 49 umeongeza upatikanaji wa maji katika eneo la Mabalizi kutoka asilimia 44 hadi 95 ambapo wateja 9,985 wameunganishwa na huduma ya maji kutoka wateja 5,436 wa awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!