Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Samia kupenya uenyekiti CCM? Mangula apambana
Habari za SiasaTangulizi

Samia kupenya uenyekiti CCM? Mangula apambana

Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mzee Phillip Mangula, amewaomba wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho, kumchagua Rais Samia Suluhu Hassan, kuwa mwenyekiti wa chama hicho. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mzee Mangula ametoa wito huo leo Ijumaa tarehe 30 Aprili 2021, jijini Dodoma, saa kadhaa kabla ya wajumbe hao kufanya uchaguzi huo.

Mkutano huo maalum wa CCM umeitishwa kwa ajili ya kujaza nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho, iliyoachwa wazi na Hayati Dk. John Magufuli, aliyefariki dunia tarehe 17 Machi 2021, ambapo Rais Samia, alipitishwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), kugombea nafasi hiyo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mzee Mangula aliwaomba wajumbe hao kumchagua Rais Samia kuwa mwenyekiti wa CCM, akisema kwamba ana uwezo wa kukiongoza chama hicho, kwa kuwa ana uzoefu kutoka kwa Dk. Magufuli.

Philip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa Ccm

Amesema, Rais Samia alizunguka katika Uchaguzi  Mkuu wa 2015 na 2020, kuinadi Ilani ya chama hicho, ambapo yeye alikuwa mgombea mwenza huku Dk. Magufuli akiwa mgombea wa Urais wa Tanzania.

“Wakati wa kuomba uongozi 2015 ndiyo awamu ya tano imeingia madarakani, kulikuwa mgombea na mgombea mwenza na walizunguka nchi nzima kutangaza mambo ambayo CCM kingeyafanya katika miaka mitano hiyo (2015-2020),” amesema Mzee Mangula.

Mwanasiasa huyo mkongwe Tanzania amesema “wawili hawa walikuwa ni Dk. Magufuli kama mgombea na mgombea mwenza akiwa Samia, katika kipindi cha miaka miaka mitano walifanya kazi nzui sana , kwa uthibitisho, ilipoingia 2020 wawili hawa waliungwa mkono na wapiga kura kwa asilimia zipatazo 85.”

Amesema, kutokana na uongozi mzuri wa Dk. Magufuli na Samia, Watanzania waliwachagua tena kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.

“Maana yake ni kwamba wananchi waliikubali kazi yao wanayoifanya wawili hao, pia wabunge katika majimbo yao walitangaza nini chama kingefanya awamu ya tano, ndio maana wabunge katika majimbo yao walishinda na kuwa wabunge kwa kutangaza ahadi ya CCM ni zaidi ya asilimia 90 ya majimbo yote,” amesema Mzee Mangula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!