Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia kuhusu bei ya mafuta: Ni tatizo la dunia nzima
Habari za Siasa

Samia kuhusu bei ya mafuta: Ni tatizo la dunia nzima

Spread the love

 

WANANCHI wa Mbalizi mkoa wa Mbeya nchini Tanzania amemuhoji Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta ambapo amewajibu kuwa licha ya jitihada za Serikali kuweka ruzuku, bei ya mafuta imekuwa ni tatizo la dunia nzima. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Rais huyo ameyasema hayo leo Ijumaa tarehe 5 Agosti akizungumza na wananchi wa eneo hilo ambapo amesema tatizo hilo litaendelea hadi dunia itakapoacha kupigana na bei za mafuta kushuka katika soko la dunia.

Vinginevyo amesema Serikali italazimika kukata fedha za miradi ya maendeleo na kuzipeleka kuweka ruzuku ili bei ya mafuta isiendelee kupanda.

“Mafuta ya magari yanaendelea kupanda bei duniani, hatua tuliyochukua kama Serikali ni kutafuta ruzuku ya kushusha bei ya mafuta, tungeachia mafuta yapande bei kama yanavyokwenda duniani mafuta yasingenunulika,” amesema Samia.

Amesema Serikali inatoa Sh 100 bilioni kila mwezi kama ruzuku kwenye mafuta ili bei zisiendelee kupanda, “mpaka huko duniani waache kupigana, mpaka huko duniani bei zianze kushuka ndiyo tutapata unafuu.”

Amesema bei ya mafuta inaendelea kupanda duniani, “lakini sisi tunashusha kwa kutoa ruzuku na Serikali ipo macho tunafanya kuhakikisha bei isipande kiasi kile kilichopanda kwa wenzetu.”

Amesema kwenye nchi zingine za Afrika Mashariki mafuta “hayanunuliki, lakini marais wote tunajitahidi kwa njia yeyote kila mmojakwa namna yake kupunguza bei ya mafuta, bei ya mafuta ni tatizo la ulimwengu mzima tunajitahidi bei zibakie pale zilipo kwa hiyo kuhusu mafuta Serikali yenu tunahangaika.”

Bei ya mafuta imepanda tena mwezi huu na kuivuka ile ya Julai 2022, ambapo petroli imepanda kwa Sh190 kwa kila lita na Sh 179 kwa kila lita ya dizeli huku mafuta ya taa yakipanda kwa Sh 323 kwa kila lita katika jiji la Dar es Salaam.

Kwa mkoa wa Mbeya bei ya petroli ni Sh 3,533, dizeli Sh 3,445 na mafuta ya taa Sh 3,888 ikiwa ni bei baada ya ruzuku.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!